• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KASI ya magonjwa yasiyopewa kipaumbele yapungua Ruvuma

Tarehe ya kuwekwa: October 15th, 2018

MKOA WA RUVUMA WAFANIKIWA KUPUNGUZA KASI YA KUENEA  MAGONJWA YALIYOKUWA HAYAPEWI KIPAUMBELE

Mkoa wa Ruvuma umefanikiwa  kupunguza kiwango cha maambukizi ya magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kutokana na mwitikio mzuri wa jamii kutumia dawakinga.

Mafanikio haya yameelezwa leo(Jumamosi) na Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme wakati akifungua semina ya uraghibishi na uhamashishaji waa viongozi wa mkoa na Halmashauri mjini Songea kuhusu kuweka mkakati wa kuyakabili magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele.

Amesema mkoa wa Ruvuma umekuwa ukikabiliana na magonjwa matano yaliyokuwa hayapewi kipaumbele ambayo ni Minyoo tumbo,Kichocho,Trakoma ,Usubi,Matende na Mabusha (Ngirimaji) katika Wilaya zote.

“Taarifa za Wizara ya Afya zinaonyesha kuwa mkoa wetu wa Ruvuma umeweza kupunguza kiwango cha maambukizi kwa magonjwa ya Trakoma,Matende na Mabusha “ alisema Mndeme

Mkuu wa Mkoa Mndeme amewapongeza Wananchi kwa kuitikia wito wa kumeza dawa kupitia kampeni mbalimbali zilizoratibiwa tangu mwaka 1998 serikali ilipoanzisha kampeni ya kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele.

Akitoa mada  Afisa Mpango Magonjwa Yaliyokuwa Hayapewi Kipaumbele Bw.Oscar Kaitaba amesema sababu za kusitisha utoaji dawa za Trakoma ,matende na Mabusha kwenye Halmashauri za Wilaya ya Songea,Namtumbo na Tunduru ni kutokana utafiti kuonyesha maambukizi kuwa chini ya asilimia moja.

Kuhusu ugonjwa wa Usubi ,Afisa Mpango Magonjwa  Yaliyokuwa Hayapewi Kipaumbele toka Wizara ya Afya Bw.Oscar Kaitaba amesema mkoa wa Ruvuma unafanya vizuri katika kutokomeza ugonjwa huu na hasa Wilaya ya Tunduru.

“Taarifa nilizonazo nazo ni kwamba Wilaya hiyo inasubiri maelekezo ya Shirika la Afya Duniani ili waweze kusitisha unywesheshaji wa dawa za kutokomeza ugonjwa wa usubi.” Alisema Kaitaba

Kwa upande wake Mratibu wa Mkoa wa Magonjwa yaliyokuwa hayapwei kipaumbele Dkt,Charles Hinju ametoa takwimu  za mkoa zinazonyesha kuwa mwaka 2016 jumla ya watu 1,052,907 kati ya 1,420,317 walipata kingatiba sawa na asilimia 74 huku kwa mwaka 2017 watu 1,192,390 kati ya 1,413,751 walipata kingatiba sawa na asilimia 84.

 Uwepo wa magonjwa yasiyopewa kipaumbele katika mkoa wa Ruvuma umekuwa na madhara mengi kama kusababisha ulemavu,upofu wa kudumu,kupunguza rasilimali fedha kwa mahitaji ya dawa na unyanyapaa kwa wagonjwa

Imetolewa na

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Ruvuma

Songea

14 Octoba,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa