• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KAYA 7045 zajiunga na CHF Songea

Tarehe ya kuwekwa: May 11th, 2018

HALMASHAURI ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma imekuwa ikitekeleza shughuli za Mfuko wa wa Afya ya jamii (CHF) tangu mwaka 2006 ambapo shughuli za kuhamasisha jamii kujiunga na CHF zimefanyika katika kata zote 21.

Kaimu Mganga Mkuu wa Manispaa ya Songea Dk.Mameritha Basike amesema hadi kufikia machi 2018, kaya 7045 sawa na asilimia 16 zilikuwa zimejiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF). 

 Dk.Basike amebainisha kuwa utoaji wa vitambulisho bure kwa wazee wenye umri wa kuanzia miaka 60 umefanyika kwa wazee 1,200 sawa na asilimia 10.9

“Kata tisa  ambazo ambazo wazee wamenukaifa na vitambulisho hivyo ni Mjini, Misufini, Majengo, Bombambili, Matogoro, Lizaboni, Matarawe, Mateka na  Seedfarm lengo likiwa ni kuwafikia wazee 11,678 katika Kata zote 21’’,anasisitiza.

Hata hivyo amesema wazee wote ambao hawajafikiwa na kupatiwa vitambulisho maalumu vya matibabu, watatambuliwa kwa vitambulisho vya kupigia kura.

Amesema Halmashauri imeingia mkataba na vituo vya kutolea huduma za afya ambavyo vinamilikiwa na Mashirika ya dini ili kutoa mitibabu bure kwa wazee 600 waliopo katika Manispaa hiyo.

 Anazitaja changamoto za Mfuko wa Afya ya jamii kuwa ni ya kukosekana kwa vituo vya serikali vya kutolea huduma za afya kwa baadhi ya maeneo na sehemu nyingine vipo vituo vya taasisi za dini ambavyo kwa taratibu zao hawapokei au hawatoi huduma hiyo hali  ambayo inachangia ugumu wa kuhamasisha jamii kujiunga na mfuko wa Afya ya jamii.

Hata hivyo Halmashauri inaendelea kufanyia kazi changamoto hiyo ili kuwezesha vituo vya Dini kutoa huduma hiyo kwa ufasaha na kuhamasisha Wananchi kuanzisha ujenzi kwa maeneo ambayo vituo vya Serikali vipo mbali na mitaa yao. Kulingana na takwimu za wazee za mwaka 2016,Manispaa ya Songea  ina zaidi ya wazee 11,000.

Imeandaliwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manipaa ya Songea

Mei 11,2018

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa