• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA MBOLEA DUNIANI.

Tarehe ya kuwekwa: October 13th, 2021

NA,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

13.10.2021

Waziri wa Kilimo nchini Tanzania Profesa Adolf Mkenda  ameongoza mamia ya Wananchi mkoani Ruvuma katika kuadhimisha siku ya mbolea duniani iliyofanyika leo tarehe 13 Oktoba 2021 katika uwanja wa Majimaji.

Mkenda alianza kwa kuwapongeza wakulima wa Mkoa wa Ruvuma kwa kuwa kitovu cha uzalishaji wa mazao ya chakula nchini hasa zao la mahindi kwa wingi na kuchangia kwa asilimia kubwa upatikanaji wa chakula kwa wananchi wa Tanzania.

Aliongeza kuwa ni muhimu kutumia siku hii ya mbolea duniani katika kuhimiza matumizi bora na sahihi ya mbolea ili kuleta tija katika maendeleo ya kilimo nchini lakini pia kwa wakulima wenyewe, hii ni kutokana na changamoto ya tija ndogo katika uzalishaji wa mazao ambapo sekta ya kilimo inachangia asilimia 15% tu katika pato la Taifa.”Alibainisha”

“Moja ya hatua sahihi ya kuongeza tija katika sekta ya kilimo ni kuhimiza matumiza sahihi ya mbolea kwa kiwango cha kutosha katika uzalishaji wa mazao yote ya chakula na biashara” Alisisitiza.

Aliendelea kwa kusema kuwa changamoto kubwa iliyopo sasa kwa wakulima ni kupanda kwa bei ya mbolea duniani na Tanzania kwa ujumla ambapo bei ya mbolea ya kuoteshea (DAP) kwa mfuko wa Kilogram 50 ni Tsh. 100000/= ukilinganisha na bei ya mwaka jana 2020 ambapo ilikuwa ni Tshs 48000/= hadi Tshs 65000/= katika maeneo tofauti nchini.

Mkenda alieleza sababu ya kupanda kwa bei ya mbolea duniani ni kutokana na janga la ugonjwa wa UVIKO 19 katika kipindi cha mwaka 2020/2021 hali iliyosababisha kupungua kwa uzalishaji wa mbolea viwandani na kusababisha ongezeko la uhitaji wa pembejeo hiyo pamoja na ongezeko la bei duniani kote ambapo hadi sasa matumaini ya kushuka kwa bei hizo bado hayajaonekana.

Hata hivyo Serikali imeamua kuchukua hatua mbalimbali ili kuhakikisha inapunguza makali ya upatikanaji wa mbolea kwa wakulima nchini kwa kufuta utaratibu wa kuagiza mbolea kutoka nje ya nchi kwa kutumia wazabuni na hivyo kutoa fursa kwa kila mfanyabiashara mwenye uwezo wa kuagiza mbolea bora na kuzileta nchini ili kusaidia ongezeko la upatikanaji wa mbolea kwa wingi. “Alieleza”

Ametoa wito kwa kampuni zote za mbolea nchini kuwaagiza mawakala wao kuhakikisha hawaongezi gharama za bei ya mbolea ili kujitengenezea faida kubwa badala yake waweke gharama nafuu ili kumsaidia mkulima kununua pembejeo hiyo.

Siku ya mbolea duniani huadhimishwa kila mwaka tarehe 13 Oktoba ikiwa ni kumbukizi ya uvumbuzi wa kirutubishi aina ya Amonia kinachopatikana hewani uliofanywa na mwana sayansi kutoka nchini Uingereza Fritz Haber mwaka 1908, na iliadhimishwa kwa mara ya kwanza duniani tarehe 13 Oktoba 2016 nchini Uingereza kwa lengo la kuelimisha umma kuhusu faida na matumizi sahihi ya mbolea.

Kauli mbiu katika maadhimisho hayo ni; “TUMIA MBOLEA BORA KWA TIJA NA KILIMO ENDELEVU”

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa