• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KIONGOZI wa Mbio za Mwenge wa Uhuru agawa vyandarua kwa wenye ulemavu

Tarehe ya kuwekwa: June 10th, 2018


KIONGOZI wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2018 Charles Kabeho amegawa  vyandarua  kwa wenye ulemavu wa viungo wapatao  20 wa kata ya Mshangano, wakiwa ni wawakilishi wa wenye ulemavu wenzao 600 wa  kata 20 za Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.

Ugonjwa wa malaria ni miongoni mwa magonjwa 10 yanayowasumbua watu wengi katika Manispaa ya Songea,hususani akina mama wajawazito, na watoto chini ya miaka mitano.Mwaka 2017 Manispaa ya Songea ilikuwa na wagonjwa wa malaria waliopata matibabu ya nje 48,252 ambao ni sawa  na asilimia 19 ya wagonjwa wote 250,038 waliopata matibabu ya nje. Wagonjwa waliougua ugonjwa na Malaria na kulazwa walikuwa 3,890 sawa na asilimia 12.8 ya wagonjwa wote 30,193 waliolazwa.

Watoto chini ya umri wa miaka mitano waliougua ugonjwa wa Malaria na kutibiwa matibabu ya nje walikuwa 17,231 sawa na asilimia 19 ya wagonjwa wote 89,861 chini ya miaka  mitano. Watoto 1,586 waliolazwa kutokana na ugonjwa wa Malaria ni sawa na asilimia 24.3 ya watoto 6,520 waliolazwa kutokana na magonjwa mengine yote.

Aidha vifo vilivyotokea dhidi ya ugonjwa wa Malaria kwa mwaka 2017 ni 99 sawa na asilimia 29 ya vifo vyote 341 vilivyotokea kutokana na magonjwa mengine. Watoto chini ya miaka mitano waliokufa kutokana na ugonjwa wa Malaria ni 43 sawa na asilimia 18 ya vifo vyote vilivyotokea kwa watoto chini ya umri wa miaka mitano ambao ni 244.

Katika kuendeleza mapambano dhidi ya ugonjwa wa malaria, Manispaa imejiwekea mikakati ifuatayo;Kushirikiana na Serikali kuu kuendesha zoezi la mpango wa ugawaji vyandarua shuleni, kwa kina mama wajawazito na watoto wanaopata chanjo ya surua umri wa  miezi tisa. kuendelea kununua dawa na vipimo vya Malaria (MRDT). Utoaji wa Elimu kuhusu kutumia vyandarua, kupima kabla ya kutibiwa, kuwahi matibabu mara unapoona dalili za malaria, kuwahi kliniki kwa mama mjazito na  kuweka mazingira katika hali ya usafi.

Halmashauri ya Manispaa ya Songea inatekeleza mpango wa kuua viluwiluwi vya mbu kwenye mazalia. Kwa mwaka 2017 Halmashauri ilipokea dawa jumla ya lita 1,000 kutoka Serikali kuu ambayo imepuliziwa kwenye mazalia ya wazi, madimbwi mita za mraba 32,000 na mazalia yaliyofunikwa mita za ujazo 50,000. Mpango huu ni endelevu katika manispaa ya Songea.

Imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Juni 11,2018


Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa