• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Kituo cha Afya Kata ya Lilambo kilichojengwa kwa Mil. 500 Chaanza kutoa Huduma za Kitabibu

Tarehe ya kuwekwa: January 3rd, 2023

Wananchi wa kata ya Lilambo Manispaa ya Songea wametoa shukrani kwa Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kujenga kituo cha Afya  ambacho kimejengwa kwa gharama ya shilingi Mil.500 fedha zilizotokana na Makusanyo ya mapato ya ndani.

Hapo awali wananchi wa kata ya Lilambo  walikuwa wanapata huduma za afya katika Zahanati na walipohitaji kupata huduma kubwa za matibabu walilazimika kutembea kwa umbali  mrefu au kukodi usafiri kwa gharama kubwa kuelekea Hospitali kubwa jambo ambalo lilikuwa kero kwa wananchi lakini baada ya kujengwa kituo  na kuanza kutoa huduma za awali kituoni hapo,  wananchi wameondolewa  adha zilizojitokeza hapo awali. “ Wananchi wameshukuru”

Hayo yamejili jana tarehe 02 Januari 2023 katika uzinduzi wa utaoaji wa huduma za awali za matibabu katika kituo cha afya Lilambo kwa lengo la kuondoa kero na kusongeza huduma kwa wananchi.

Mkuu wa Idara ya Mipango na Uratibu  Manispaa ya Songea Andambike Kyomo alisema “Ukamilishaji wa kituo hicho umetumia miongozo ya Wizara ya Afya TAMISEMI  pia  ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi wa Chama Cha Mapinduzi CCM ambayo imeelekeza kutatua kero za wananchi na kusogeza huduma bora kwa jamii.”  Alisisitiza”

Kyomo aliongeza kuwa Kituo hicho kimejengwa kwa gharama ya shilingi Mil. 500 fedha kutoka mapato ya ndani  pia ni utekelezaji wa maelekezo ya Mheshimiwa Waziri Mkuu kuwa kila Halmashauri ijenge  kituo cha afya kupitia mapato yao ya ndani ya Halmashauri.

Mafanikio hayo yametokana na ushirikiano wa karibu na viongozi ngazi ya Mkoa, Wilaya, Mbunge, Wakuu wa Idara na Vitengo, Watendaji wa kata na Mitaa, Waheshimiwa Madiwani na wananchi kwa ujumla na kufikia hatua ya kukamilisha ujenzi na kuanza kutoa huduma za awali za matibabu kwa wananchi. Kyomo alishukuru."

Kwa upande wake Mheshimiwa Diwani kata ya Lilambo Yobo Mapunda alianza kwa kutoa shukrani kwa uongozi na wananchi kwa kufanikiwa kujenga kituo cha afya na kuanza kutoa huduma za awali kwa wananchi ambapo itawasaidia wananchi kuwa punguzia adha ya kutembea mwendo mrefu kufuata matibabu . “alishukuru”

Yobo alibainisha kuwa kituo cha afya Lilambo  tayari tumepokea waganga wawili 2 na wahudumu wa afya watatu 3 kwa ajili ya kuanza kutoa huduma za kitabibu ambapo kwasasa huduma zitakazotolewa ni huduma za awali na baada ya kukamilika kwa miundombinu na vitendea kazi huduma nyingine zitatolewa.

Naye kaimu mganga Mkuu Manispaa ya Songea Beda Mgegedu alisema aina ya matibabu yatakayoanza kutolewa katika kituo hicho ni huduma za awali (OPD na maababra na baada ya kukamilika kwa taratibu nyingine huduma kubwa za matibabu zitatolewa.

 

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.



Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa