• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KITUO KIKUU CHA MABASI SHULE YA TANGA SONGEA CHA FUNGULIWA RASMI 10.03.2020

Tarehe ya kuwekwa: March 6th, 2020

Mstahiki Meya Manispaa ya Songea Alhaji Abdul Hassani Mshaweji, amesema  “Maendeleo ya Nchi hayawezi kuja bila uwekezaji”.

  Kauli hiyo imetolewa katika kikao cha Wadau wamiliki wa Vyombo vya usafirishaji abiria,Viongozi wa Wasafirishaji abiria Mkoa wa Ruvuma(UWARU), pamoja na wadau wa usafirishaji ambao ni (RTO), LATRA, TARURA, Kilichofanyika tarehe 02/03/2020 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Mshaweji alisema Ujenzi wa Stendi ya shule ya Tanga umekamilika na sasa iko tayari kwa ajili ya kuanza kutoa huduma ikiwa pamoja na Halmashauri kuanza kukusanya mapato kupitia Stendi hiyo. Alisema Stendi hiyo ina jumla ya Vibanda 50, ikiwa Vibanda 30 ni Vibanda kwa ajili ya shughuli za biashara na  Vibanda 20 ni kwajili ya kukatia tiketi za mabasi.  

Alisema, “ makubaliano yaliyofanyika na wadau wote kwa stendi zote (4) ni pamoja Mabasi yaendayo Dar es salaam, Njombe, Iringa, Mbeya, Sumbawanga, Dodoma,kupitia barabara ya Njombe safari zao zitaanzia Stendi ya Tanga na zinaporejea safari zake zitaishia stendi kuu ya Tanga.

Mabasi yaendayo kupitia barabara ya Lindi kwenda Dar es salaam, Lindi, Mtwara, Tunduru yataanzia  Stendi ya Tanga kupitia Stendi ya Msamala na Seedfarm, na yanaporejea yatapitia Stendi ya Seedfarm kuishia stendi ya Msamala.

Mabasi yanayoelekea njia ya Mbinga, Nyasa,  na Songea vijijini safari zake zitaanza Stendi ya Msamala kupitia stendi Mfaranyaki kwa dakika 10 tu, na yanaporejea yatapitia Mfaranyaki na kuishia safari zake stendi ya Msamala. Pia daladala zote za Mshangano, Tanga, Mlilayoyo zitaanza safari stendi ya Mfaranyaki kupitia Msamala, Tanga na kuelekea zinakomalizia safari zake.

Aidha, Mabasi yaendayo Makambako na Njombe yatapitia stendi kuu Tanga na kumalizia safari zake Stendi Msamala. Pia Mabasi yanayotokea barabara Lindi yaendayo Mbeya , Njombe na Iringa yataruhusiwa kuingia katikati ya Mji kama yatakuwa na Abiria au kujaza Mafuta.

Aliongeza kuwa magari yanayotoka  maeneo ya Matimila,Mletele, Ngwinde, na Chengena safari zao zitaanzia kituo cha Daladala cha Majengo- -Mitumbani na kumalizia safari zake katika kituo hicho. Pia Magari yaendayo Mpitimbi ,Mkenda, Muhukuru, Namatuhi, Ndongosi na Namabengo zitaanzia kituo cha daladala majengo—mitumbani  na kumalizia kituo hicho.

Naye Mratibu wa Polisi  Mkoa wa Ruvuma  SP  Salumu Morimori aliseama” kazi ya Jeshi la polisi ni kusimamia Sheria na Taratibu zilizowekwa na Serikali,  hivyo aliwaasa wamiliki wa Vyombo vya Moto na Madereva kufuata makubaliano haya ambayo mmeyapitisha na atakaye kwenda kinyume na makubaliano haya atachukuliwa hatua za kisheria ikiwemo na kupelekwa mahakamani.”Alisisitiza.

 

                                                             IMEANDALIWA NA;

                                                                 AMINA PILLY

                                        KAIMU AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bil. 22.9 Kujenga Masoko ya Kisasa Manzese A na B, na Kiwanda cha Kuchakata Mazao ya Nafaka Lilambo

    July 06, 2025
  • MBUNGE SONGEA MJINI AKABIDHI KOMPYUTA NA KUFADHILI UKARABATI WA OFISI ZA POLISI

    June 27, 2025
  • DC Songea bAzindua Dawati la Huduma za Ustawi wa Jamii Stendi ya Mabasi Songea

    June 24, 2025
  • Meya Mbano; Amewataka Wananchi Kulinda Haki za Watoto

    June 16, 2025
  • Tazama zote

Video

Makabidhiano ya Mkataba Soko la Manzese A&B
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa