• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KIWANGO cha zebaki Mto Ruvuma kinatishiaTanzania na Msumbiji

Tarehe ya kuwekwa: May 27th, 2018

KUELEKEA maadhimisho ya siku ya mazingira duniani ambayo yanaanzia Mei 30 na kilele chake Juni 5 kila mwaka,uchafuzi wa mto Ruvuma unaofanywa na wachimbaji wa madini katika nchi ya Tanzania na Msumbiji unatishia ustawi wa viumbehai wakiwemo binadamu na viumbehai wa majini na ardhini.

Afisa Maliasili wa Mkoa wa Ruvuma Afrikanus Challe anasema wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu wanatumia mito inayomwaga maji yake mto Ruvuma kusafishia  dhahabu kwa kutumia kemikali ya zebaki ambayo inaingia moja kwa moja hadi mto Ruvuma.Anaitaja mito midogo inayomwaga maji yake mto Ruvuma ambayo inaongoza kwa uchafuzi kuwa ni mto Lunyere na Lumeme kwa upande wa Tanzania na mito ya Msinje na Kipingi ambayo inaanzia nchini Msumbiji.

Challe anasema machimbo ya dhahabu katika maeneo ya Kizito,Mpepo,Ndondo,Luporo,Liumbe na Manyigu katika nchi za Tanzania na Msumbiji yapo kwenye vyanzo vya maji vya mito hiyo ambayo inamwaga maji yake katika mto Ruvuma ambao unamwaga maji yake Bahari ya Hindi.

“Wachimbaji toka nchi zote mbili wanafanya shughuli zao za uchimbaji bila tahadhari na kufuata kanuni na sheria za uchimbaji matokeo yake wanafanya uchafuzi ulisababisha mto Ruvuma kuathirika kwa kiwango kikubwa na kemikali za zebaki’ na takataka nyingine’,anasisitiza Challe.

Challe anashauri shughuli zote za uchimbaji jirani na vyanzo vya maji zinatakiwa kuzuiwa na nchi zote mbili kwa kuwa vipimo vya maabara vinaonesha kuwa mto Ruvuma una kiwango kikubwa cha zebaki ambacho kinaweza kuathiri binadamu na viumbehai.

Kwa mujibu wa matokeo ya maabara kwenye vyanzo vya maji vya Songeapori mkoani Ruvuma vilivyochukuliwa  vinaonesha kuwa chanzo hicho ambacho kinamwaga maji yake mto Ruvuma kina kiwango kikubwa cha zebaki ambacho ni 0.02(Hg) ambapo kiwango cha kawaida kinachokubalika ni 0.005(Hg).

Vipimo vya maabara za uchunguzi wa  maji vilivyochukuliwa kati ya mwaka 2008 hadi 2010 ,vilibaini kuwa maji hayo licha ya kuwa na kiwango kikubwa cha zebaki,pia yana kiwango kikubwa cha taka/tope(turbidity) ambacho kinavuka kiwango kinachokubalika kitaifa na hata cha Shirika la Afya Duniani (WHO).

Kiwango cha taka ambacho kinakubalika kitaifa kinaelezwa kitaalam kuwa ni etu 30; kiwango cha kimataifa ni etu 5 – 25. Lakini maji ya chanzo hicho yana etu 1,141 jambo ambalo ni hatari.

“Hali ni mbaya zaidi kwenye maeneo ambayo mito inatoka machimboni na imeungana na mto Ruvuma hasa wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma na Mkoa wa Mtwara,katika maeneo hayo mtu akila kuanzia samaki wanne wenye zebaki anaweza kuathirika kwa kuwa kemikali hiyo ni sumu’’,anasisitiza Challe.

Mwandishi wa Makala haya ni Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Baruapepe:albano.midelo@gmail.com,simu 0784765917


Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa