• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MAADHIMISHO ya siku ya mazingira kufanyika kesho Songea

Tarehe ya kuwekwa: June 4th, 2018

KESHO ni kilele cha maadhimisho ya Juma la mazingira ambayo kimkoa yanatarajia kufanyika katika Mtaa wa Mjimwema B Kata ya Mjimwema Manispaa ya Songea,ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme.Kila mwaka wiki ya mazingira inafanyika kuanzia Mei 31 na kilele chake ni Juni 5.Kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni "Mkaa ni Gharama,Tumia Nishati Mbadala".Madhumuni ya ujumbe huu kitaifa unalenga kuelimisha matumizi ya nishati mbadala kwa wananchi ili kukabiliana na changamoto ya ukataji miti hovyo.

Wakati tunaadhimisha kilele cha siku ya mazingira,Uchafuzi na uharibifu wa mazingira ardhini,majini na nchi kavu umekithiri katika kiwango ambacho kinatishia kutoweka kwa sayari ya Dunia na viumbehai, endapo hatua za makusudi hazitachukuliwa kuinusuru hali hiyo.

Athari za mabadiliko ya hali ya hewa hapa nchini na duniani kote zinasababisha kila mwaka serikali kutenga bajeti ya zaidi y ash.trilioni 1.12 kukabiliana na athari za mazingira kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa.

Kasi ya kutoweka kwa maji inaongezeka,tatizo la upatikanaji wa maji pia linaongezeka kutokana na kuongezeka kwa ukame unaosababishwa na shughuli za kibinadamu kwenye vyanzo vya maji.Tusipochukua hatua,Vita ya Dunia ya kugombania majii inakuja.

Wanasayansi wanasema shughuli mbalimbali za kibinadamu zimesababisha kuongezeka kwa joto la Dunia kwa nyuzi 0.85c na kusababisha madhara yote yanayotokea hivi sasa duniani yakiwemo ukame,magonjwa,mafuriko na mabadiliko ya tabianchi.

Hata hivyo wanasayansi wanatahadharisha kuwa iwapo joto  duniani litaongezeka  hadi kufikia nyuzi joto 1.5c ambalo ni ongezeko la  nyuzi joto 0.65c  viumbehai  wote waliopo duniani hawataweza kumudu  kuishi na hiyo itakuwa ndiyo mwisho wa vita kuu ya tatu ya Dunia ambayo itaangamiza Dunia nzima na viumbehai waliopo.

Kwa mujibu wa wanasayansi Mwaka 2012  ongezeko la joto duniani lilikuwa nyuzi 0.7c na kwamba kiwango cha joto kilifikia nyuzi 0.85c hadi kufikia mwaka 2015.

Moja ya sababu kuu zinazochangia kuendelea kuongezeka kwa hewa ya ukaa angani ni maendeleo ya viwanda ambavyo vinatoa moshi ambao unasambaa angani na kufanya uchafuzi mkubwa wa mazingira ya anga pamoja na moshi mwingi wa magari  husababisha gesi ya ukaa kwenda moja kwa moja angani.

Utafiti mpya umeonesha kuwa watu milioni sita kote duniani wanakufa kila mwaka kutokana uchafuzi wa  mazingira ya hewa ambapo asilimia 90 ya watu wote duniani wanavuta hewa chafu.

Ripoti ya Shirika la Afya Duniani (WHO) iliyotolewa Septemba 2016, inaeleza kuwa watu 9 kati ya 10 wanavuta hewa chafu duniani kote kila siku,hali inayoongeza hatari ya watu kuugua magonjwa mbalimbali yanayosababisha vifo vingi.

Mazingira  salama ndiyo msingi wa uhai wetu,mazingira yakiwa na afya tutakuwa na afya,mazingira yakiugua tutaugua na mazingira yakifa viumbe wote tunafutika  katika uso wa dunia.

Makala haya yameandaliwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Juni 4,2018


Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa