• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MAADHIMISHO YA SIKU YA MWANAMKE ANAYEISHI KIJIJINI 2021

Tarehe ya kuwekwa: October 15th, 2021

NA,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

15.10.2021.

Halmashauri ya Manispaa ya Songea imeungana na Watanzania wengine katika kuadhimisha siku ya Mwanamke anayeishi Kijijini leo tarehe 15 Oktoba 2021.

Maadhimisho hayo yamefanyika katika kata ya Mwengemshindo Manispaa ya Songea na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoka ndani ya Manispaa ya Songea wakiwemo Waheshimiwa Madiwani pamoja na Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Songea.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa ni Mstahiki Meya Manispaa ya Songea Michael Mbano ambaye alianza kwa kuwapongeza viongozi wa Manispaa ya Songea kwa kuratibu maadhimisho hayo ambayo yamefanyika kwa mara ya kwanza nchini Tanzania ambapo kitaifa yameadhimishwa Mkoani Kilimanjaro.

Mbano amewataka wanaume wote  kuachana na mila na desturi potofu zinazowazuia wanawake hasa wanaoishi Kijijini kumiliki ardhi, kwa kuwaruhusu na kuwarithisha watoto wa kike haki sawa na vijana wa kiume katika suala zima la kumiliki ardhi kama hazina ya maisha yao ya baadae.

Amesisitiza kuwa maadhimisho haya yamelenga kufanya kampeni ya kumuwezesha mwanamke hasa anayeishi kijijini kuwa na haki ya kumiliki ardhi pamoja na kutoa nafasi ya pekee kwa mwananmke katika kukabiliana na ugonjwa wa UVIKO 19.”Alibainisha”

Amewataka wanawake kutumia nafasi yao kama fursa katika kukabiliana na ugonjwa wa UVIKO 19 kwa kuanza kutoa elimu kwenye familia zao  namna ya kujikinga na kuandaa vifaa kinga kama vile maji tiririka, vitakasa mikono pamoja na barakoa n.k.

Ametoa wito kwa wanawake na wananchi wote wa Manispaa ya Songea kuendelea kujitokeza kwa wingi kupata chanjo ya Uviko 19 na amewatoa hofu  wananchi kuhusiana upotoshaji wa jamii juu ya matumizi ya  chanjo hiyo na  kuwahakikishia usalama na umuhimu wa kutumia chanjo ili kujikinga na ugonjwa wa UVIKO 19.’Alisisitiza’ 

Naye Afisa maendeleo ya jamii Manispaa ya Songea Joyce Mwanja alibainisha kuwa, lengo la kuadhimisha siku hii ni kuwawezesha wanawake wanaoishi kijijini katika kukabiliana na changamoto ya UVIKO 19 pamoja na kuelimisha jamii juu ya haki ya mwanamke katika umiliki wa ardhi.

Aliongeza kuwa Wizara ya Maendeleo ya jamii, Afya, Jinsia, wazee na Watoto imeandaa siku hii maalumu ili kuelimisha jamii iweze kutambua nafasi ya mwanamke katika kukabiliana na UVIKO 19 kwa kutoa elimu na kuhamasisha juu ya njia mbalimbali za kujikinga na UVIKO 19 pamoja na uchomaji  wa chanjo..

Maadhimisho hayo yaliadhimishwa na wananchi mbalimbali waliojitokeza kupata chanjo ya UVIKO 19 uwanjani hapo wakiongozwa na Diwani wa Kata ya Mwengemshindo Kapinga Osmund Sixmund.

Kauli mbiu katika maadhimisho ya Siku ya mwanamke anayeishi kijijini ni;

“TUJENGE USTAHIMILIVU KWA MWANAMKE ANAYEISHI KIJIJINI KATIKA KUKABILIANA NA UVIKO 19”

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa