• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MADHUMUNI ya kusaini Mkataba wa Lishe Manispaa ya Songea

Tarehe ya kuwekwa: November 5th, 2018

MADHUMUNI YA KUSAINI MKATABA YA LISHE MANISPAA YA SONGEA

TAREHE 23 OKTOBA 2018

 

UTANGULIZI


Historia ya kusaini mkataba wa lishe unaanzia tarehe. 19/12/2017 ambapo Waziri wa OR-TAMISEMI Mh. Seleman Jaffo alisaini mkataba wa UTEKELEZAJI MPANGO SHIRIKISHI WA LISHE TAIFA na Wakuu wa Mikoa wote Tanzania bara, na mnamo tarehe 24/09/2018 Mkuu wa Mkoa aliwasainisha Wakuu wa Wilaya wote kufuatia agizo la Makamu wa Rais Mh.Samia Suluhu Hassani alilotoa kwenye mkutano wa urutubishaji chakula uliofanyika Dar es Salaam kuanzia tarehe 23 hadi 24/08/2017. Hii ni katika kuongeza kasi ya utekelezaji na uwajibika katika Swala la Lishe Nchini.

Mkataba huu una malengo matatu,Vipaumbele kumi katika kufikia malengo hayo, Wilaya itakuwa na majukumu na  wajibu 17, vigezo 10 vya upimaji utekelezaji wa mkataba na viashiria 10 vya upimaji utendaji kazi. Aidha Mkoa utakuwa na majukumu na wajibu saba katika upimaji utendaji kazi wa wilaya. Haya yote yameainishwa kwenye Mkataba huo.

 Mkataba huu utakuwa wa muda wa miaka minne na utaanza tarehe 01 Julai, 2018 hadi tarehe 30 Juni, 2021. Aidha, Mkataba huu utapimwa kila mwisho wa mwaka husika.

  • Malengo matatu ya Mkataba ni
  1. Lengo kubwa ni kufanikisha suala la kuboresha hali ya lishe na kupunguza athari za utapiamlo katika Mkoa.
  2. Kuhakikisha kuwa Mkoa unasimamia ipasavyo utekelezaji wa  afua za lishe 
  3. Kuchukua hatua madhubuti za kupunguza hali duni ya lishe katika eneo lake
  •  Kupanga na kutenga fedha kwa ajili ya kutekeleza afua za lishe katika mipango ya Mkoa na Halmashauri zilizo chini yake

  Vipaumbele kumi ili wilaya iweze  kufikia malengo yaliyoainishwa katika Mkataba huu:-

  • Kuandaa/kutenga fedha kwa ajili ya afua za lishe katika Wilaya. 
  • Kusimamia na kuhakikisha kuwa fedha iliyotengwa kwa ajili ya utekelezaji wa afua za lishe inatumika katika  Wilaya.
  • Kuhakikisha kuwa kunakuwa na Mpango jumuishi wa Lishe katika Wilaya.
  • Kuhakikisha kuwa watoto wenye umri kuanzia miezi 6 hadi miaka 5 wanapatiwa nyongeza ya matone ya Vitamini A.
  • Kuhakikisha kuwa wanawake wajawazito wanapatiwa vidonge vya madini ya chuma na Asidi ya Foliki.
  • Kuhakikisha kuwa kinamama wenye watoto walio na umri chini ya miezi 6 wanapatiwa elimu ya unyonyeshaji wa maziwa ya mama pekee kwa muda wa miezi 6.
  • Kuhakikisha kuwa kinamama wenye watoto wenye umri wa kuanzia miezi 6 hadi miaka 2 wanapatiwa elimu ya ulishaji wa vyakula vya nyongeza kwa watoto.
  • Kuhakikisha kuwa watoto wenye utapiamlo mkali wanapatiwa matibabu katika vituo vya kutolea huduma za afya.
  • Kuhakikisha kuwa Vikao vya Kamati za Lishe za Halmashauri vinafanyika na vikao vya Kamati za Maendeleo ya Kata na Vijiji/Mitaa vinaweka ajenda ya lishe kuwa ya kudumu.
  • Kuhakikisha kuwa ukaguzi wa ubora wa chakula na dawa unafanyika.

Ili wilaya iweze kutekeleza malengo hayo ina majukumu na wajibu kumi na saba kama ifuatavyo:

Kutenga fedha kwa ajili ya afua za lishe kama itakavyokuwa inaelekezwa katika mwongozo wa bajeti wa kila mwaka;

Kusimamia ajira kwa wataalam wa lishe katika Halmashauri;

Kusimamia uundwaji wa Kamati za Lishe za Halmashauri kwa mujibu wa Mwongozo uliopo na Kuhakikisha kamati za Maendeleo za Kata na Vijiji/Mitaa zinasimamia maswala ya lishe katika ngazi zao;

Kuhakikisha Kamati za Lishe za Halmashauri zinafanya vikao na kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Mwongozo;

Kusimamia na kuhakikisha sekta mtambuka zinapanga na kutekeleza afua za lishe;

Kuhakikisha kuwa Halmashauri inakuwa na Mpango Mkakati wa Lishe;

Kuhakikisha kwamba mipango ya wadau wote wa lishe inajumuishwa katika mipango ya Halmashauri (MTEFs);

Kuhakikisha kwamba masuala ya lishe yanakuwa ajenda ya kudumu kwenye vikao vyote vya kisheria katika ngazi za Halmashauri, Kata na Vijiji/Mitaa;

Kuhakikisha kwamba, taarifa za kadi alama ya lishe (Nutrition Score Card) inajadiliwa kila robo kabla ya kuwasilishwa katika ngazi husika/inayofuata na pia kutoa mrejesho na kuweka mikakati;

Kujadiliana na kutia saini Mkataba wa Utendaji Kazi;

Kuweka mazingira wezeshi ili watumishi waweze kutenda kazi zao kwa utaalamu, umakini na ufanisi ili kuchangia ipasavyo katika utekelezaji wa malengo ya Wilaya;

Kusimamia utendaji wa kila siku ili kutekeleza Sera, Mikakati na Vipaumbele vya kitaifa kulingana na Mpango jumuishi wa Lishe wa Taifa;

Kuainisha na kuwasilisha changamoto za kiutendaji zinazoikabili Wilaya na kupendekeza mikakati ya kutatua changamoto hizo katika Mamlaka zinazohusika;

Kufanya mapitio ya utendaji kazi wa Wilaya kadiri itakavyohitajika katika kutekeleza Mpango jumuishi wa Lishe wa Taifa;

Kuandaa na kuwasilisha taarifa za utendaji kazi katika Mamlaka zinazostahili kadiri itakavyohitajika kwa muda ulioainishwa;

Kufanya tathmini binafsi ya utekelezaji wa Mkataba wa Utendaji Kazi wa Wilaya kila mwisho wa mwaka na kuwasilisha taarifa katika Mamlaka zinazostahili; na

Kushiriki katika tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Utendaji Kazi wa Wilaya itakayofanywa na MKOA kila mwisho wa Mwaka.

kutakuwa na vigezo  kumi vya upimaji utekelezaji wa mkataba kama ifuatavyo:

kiasi cha fedha kilichotengwa kwa ajili ya afua za lishe kulingana na mwongozo wa bajeti wa mwaka husika.

kiasi cha fedha kilichotumika katika utekelezaji wa afua za lishe kwa mwaka husika.

wilaya kuwa na mpango mkakati wa lishe.

asilimia ya watoto wenye umri kuanzia miezi 6 hadi miaka 5 waliopatiwa nyongeza ya matone ya vitamini a

asilimia ya wanawake wajawazito waliopatiwa vidonge vya madini ya chuma na asidi ya foliki.

asilimia ya akinamama wenye watoto walio na umri chini ya miezi 6 waliopatiwa elimu ya unyonyeshaji wa maziwa ya mama pekee kwa muda wa miezi 6.

asilimia ya akinamama wenye watoto walio na umri wa kuanzia miezi 6 hadi miaka 2 waliopata elimu ya ulishaji wa vyakula vya nyongeza kwa watoto.

asilimia ya watoto waliopatiwa matibabu ya utapiamlo katika vituo vya kutolea huduma za afya.

asilimia ya vikao vya kamati za lishe za halmashauri vilivyofanyika kwa mwaka husika.

idadi ya kaguzi za ubora wa chakula na dawa zilizofanywa na kamati ya ukaguzi wa ubora wa chakula na dawa (chumvi yenye madini joto, vyakula vilivyoisha muda n.k)

                                      

Aidha kutakuwa na viashiria kumi vya upimaji utendaji kazi

asilimia ya kiasi cha fedha kilichotengwa katika bajeti kwa ajili ya afua za lishe kulingana na idadi ya watoto walio na umri chini ya miaka mitano katika halmashauri kwa mujibu wa mwongozo wa mwaka husika.

  • asilimia ya kiasi cha fedha kilichotumika kutekeleza afua za lishe ukilinganisha na kiasi cha fedha kilichotengwa katika bajeti katika halmashauri na kata.
  • uwepo wa mpango mkakati wa lishe wa halmashauri.
  • idadi ya watoto wenye umri wa miezi 6 hadi miaka 5 waliopatiwa nyongeza ya matone ya vitamini a ukilinganisha na idadi ya watoto wenye umri huo katika wilaya.
  • idadi ya wanawake wajawazito waliopatiwa vidonge vya madini ya chuma na asidi ya foliki ukilinganisha na idadi ya wajawazito wote wanaotarajiwa katika wilaya.
  • idadi ya akinamama wenye watoto walio na umri chini ya miezi 6 waliopatiwa elimu ya unyonyeshaji wa maziwa ya mama pekee ukilinganisha na idadi ya akinamama wote wenye watoto walio na umri chini ya miezi sita katika wilaya.
  • idadi ya akinamama wenye watoto wenye umri wa kuanzia miezi 6 hadi miaka 2 waliopatiwa elimu ya ulishaji wa vyakula vya nyongeza kwa watoto ukilinganisha na idadi ya akinamama wote wenye watoto wenye umri huo katika wilaya.
  • idadi ya watoto wenye utapiamlo waliopatiwa matibabu ukilinganisha na idadi ya watoto wote waliogunduliwa kuwa na utapiamlo.
  • idadi ya vikao vya kamati ya lishe vilivyofanyika ukilinganisha na idadi ya vikao 4 vinavyotakiwa kufanyika kwa mwaka husika katika halmashauri na idadi ya vikao vya kata vilivyofanyika vikiwa na ajenda ya lishe.
  • idadi ya kaguzi za chakula na dawa zilizofanyika kulinganisha na kaguzi zilizotakiwa kufanyika kwa mwaka husika katika halmashauri na kata.

 

Katika upimaji wa utendaji kazi Ofisi ya Mkuu wa Mkoa itakuwa na majukumu na wajibu saba kama ifuatavyo: -

  • Kuwezesha Wilaya kutekeleza Sera, Mikakati na Vipaumbele vya Taifa na Mkoa kulingana na Mpango jumuishi wa Lishe wa Taifa na wa Mkoa.
  • Kufanya mapitio, marekebisho na kupendekeza uhuishaji wa Mpango jumuishi wa Lishe wa Taifa utakaowezesha Wilaya kutekeleza majukumu yake na kufikia malengo
  • Kuweka mazingira wezeshi ili Wilaya itekeleze malengo yake kikamilifu
  • Kuwezesha Wilaya kupata rasilimali (watumishi, vifaa, fedha, Muda) zinazohitajika ili uweze kutekeleza malengo yake
  • Kuhakikisha rasilimali zilizotengwa kwa ajili ya Wilaya zinaifikia kwa wakati
  • Kufanya ufuatiliaji na mapitio ya utendaji kazi wa Wilaya katika vipindi vilivyokubalika
  •  Kufanya tathmini ya utekelezaji wa Mkataba huu wa Utendaji Kazi wa Wilaya kila mwisho wa Mwaka.

Wilaya itawasilisha taarifa za utendaji kazi za robo mwaka na mwaka Mkoani kabla ya tarehe 15 ya mwezi unaofuata, Aidha Iwapo utajitokeza mgogoro wowote katika utekelezaji wa mkataba huu basi pande zote mbili zitakaa pamoja ili kutatua mgogoro huo.

ASANTENI

 

 

MKURUGENZI WA 

MANISPAA YA SONGEA.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa