• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MADIWANI MANISPAA YA SONGEA WANATAKIWA KUSIMAMIA IPASAVYO MIRADI YA MAENDELEO

Tarehe ya kuwekwa: November 18th, 2021

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

18.11.2021

Madiwani Halmashauri ya Manispaa ya Songea watakiwa kushiriki katika kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika maeneo yao.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema wakati akizungumza na Madiwani hao katika kikao cha baraza la Madiwani kilichofanyika leo tarehe 18 Novemba 2021 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea kwa lengo la kujadili na kupanga mipango mbalimbali ya maendeleo ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea.

Mgema alisema kuwa katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo Madiwani wanayo nafasi kubwa kwa kusimamia na kuhakikisha kwamba miradi hiyo inatekelezwa katika maeneo yao kwa kiwango stahiki na muda maalumu uliopangwa na Serikali ambapo kwa Wilaya ya Songea miradi yote ya mpango wa maendeleo ya Taifa na mapambano dhidi ya UVIKO 19 inatakiwa kukamilika ifikapo tarehe 30 Novemba 2021.’Alisisitiza’

Naye Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea Michael Mbano alieleza kuwa miongoni mwa mikakati ya baraza hilo ni pamoja na kuboresha miundombinu ya barabara katika maeneo yaliyopo katikati ya mji ikiwemo na barabara ya mtaa wa Mahenge pamoja na kutoa mafunzo kwa Madiwani wa Manispaa ya Songea kuhusiana na mfuko wa afya ya jamii (CHF iliyoboreshwa) kwa lengo la kuongeza uelewa kwa Madiwani ili waweze kuwahamasisha wananchi kujiunga na mfuko huo.

Amewataka Madiwani wanapopanga bajeti ya maendeleo wazingatie vipaumbele vya wananchi ili kuweza kutatua changamoto zinazojitokeza katika utekelezaji wa mipango ya maendeleo katika Manispaa ya Songea.

Akijibu hoja iliyotolewa na Mheshimiwa Diwani kata ya Mletele Lungu Maurus Gerald kuhusiana na vituo vya mauzo ya mahindi, Mbano alisema kuwa hadi sasa katika Manispaa ya Songea mauzo ya mahindi yanafanyika katika kituo kimoja kilichopo Mwanamonga ambapo kila mwananchi anayetaka kuuza mahindi yake anatakiwa kupeleka katika kituo hicho.”Alibainisha”

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Songea Ally Abdallah Ally amewapongea waheshimiwa Madiwani na Viongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa kufanya vizuri na kuweza kujenga vituo vya afya vingi ambavyo ni pamoja na kituo cha afya Subira, Lilambo na Mletele ambapo vitasaidia kutatua changamoto ya ukosefu wa huduma bora za afya katika maeneo hayo.

Amewataka Madiwani kuendelea kutimiza wajibu wao kwa kuzingatia utekelezaji wa Ilani ya chama cha mapinduzi pamoja na kushiriki katika kusimamia fedha zilizotolewa kwa ajili ya mpango wa maendeleo ya Taifa na mapambano dhidi ya UVIKO 19 zinatumika kwa matumizi stahiki na hilo litawezekana kwa kudumisha ushirikiano kati yao na wataalamu hasa kwenye suala zima la utekelezaji wa miradi hiyo kwa manufaa ya wananchi wao.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bil. 22.9 Kujenga Masoko ya Kisasa Manzese A na B, na Kiwanda cha Kuchakata Mazao ya Nafaka Lilambo

    July 06, 2025
  • MBUNGE SONGEA MJINI AKABIDHI KOMPYUTA NA KUFADHILI UKARABATI WA OFISI ZA POLISI

    June 27, 2025
  • DC Songea bAzindua Dawati la Huduma za Ustawi wa Jamii Stendi ya Mabasi Songea

    June 24, 2025
  • Meya Mbano; Amewataka Wananchi Kulinda Haki za Watoto

    June 16, 2025
  • Tazama zote

Video

Makabidhiano ya Mkataba Soko la Manzese A&B
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa