• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MADIWANI MTWARA MIKINDANI WAFANYA ZIARA MANISPAA YA SONGEA.

Tarehe ya kuwekwa: December 26th, 2022

Mstahiki Meya Manispaa ya Mtwara /Mikindani   Shadida Ndile amewaongoza Madiwani katika kutembelea Manispaa ya Songea kwa ajili ya  kujifunza namna ya uendeshaji wa  shughuli mbalimbali za maendeleo ikiwemo  ukusanyaji wa mapato ya ndani ya Halmashauri.

Ziara hiyo imefanyika tarehe 23 Disemba 2022 katika  Halmashauri  Manispaa ya Songea ambapo walifanikiwa kutembelea Miradi mbalimbali ikiwemo Stendi mpya ya Mabasi Songea, Vikundi, Machinjio ya kisasa Songea pamoja na Kituo cha Afya Lilambo  kilichojengwa kwa fedha za mapato ya ndani.

Ndile alisema Ziara yao imejaa mafanikio makubwa kutokana nakujifunza namna ya ukusanyaji wa mapato kwa kuweka wasimamizi kwa kila  chanzo cha mapato ( Meneja) hali ambayo imepelekea kuongezeka kwa mapato ya Halmashauri, namna ya ukopeshaji wa mikopo kwa vikundi vya wanawake4%,  Vijana 4%, na walemavu 2%, Usimamizi bora wa miradi ya maendeleo, na matumizi sahihi ya sheria ndogo za Halmashauri.

 Amewataka Madiwani na Wataalam wote kuendelea kutoa ushirikiano katika kukusanya mapato pamoja na kuongeza  ubunifu katika  kuibua vyanzo mbalimbali vya  Mapato ndani ya Halmashauri  ili kufikia matarajio ya Serikali yaliyowekwa.

Aliongeza kuwa viongozi na wataalamu  wanapaswa kuongeza ushupavu na uimara katika kutekeleza shughuli za Serikali ambazo zitasaidia kuonesha taswira nzuri na kuleta tija ya  Maendeleo katika Halmashauri/Nchi kwa ujumla.

Naye Zuhura Mikidadi Diwani wa Viti maalmu Mtwara Mikindani alisema kupitia Ziara hiyo  amejifunza namna ya uendeshaji wa machinjio ya kisasa, utoaji wa  mikopo ya uwekezaji  kwa vikundi (uwekezaji wa viwanda vidogo)  na sio mikopo ya mtu mmoja mmoja ambayo haileti tija kwa jamii na kuahidi kutumia elimu hiyo kwa kuwafundisha wananchi wengine kupitia kata anayoiongoza.   

Kwa upande wake Ahamadi Kalikumbe (Diwani ) alisema kuwa mafanikio yanayoonekana katika kutekeleza zoezi la ukusanyaji wa mapato ni ushirikiano baina ya waheshimiwa Madiwani na wataalamu na namna ya ukopeshaji wa vikundi, na ufuatiliaji wa madeni kwa wananavikundi waliokopeshwa.

Kwa upande Mstahiki Meya Michael Mbano  alitoa shukrani na kuwakaribisha tena kuja kutembelea kwa mara nyingine kwa ajili ya  kufanya tathimini kupitia shughuli walizojifunza  ili kubaini mafanikio na changamoto wakati wa utekelezaji na usimamizi wa zoezi la ukusanyaji wa mapato kupitia vyanzo  mbalimbali ikiwemo madini, vibali vya sherehe, lessen za vileo, na utoaji wa mikopo kwa vikundi.

           

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.

  



Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa