• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MADUKA 48 YA DAWA MUHIMU YAFUNGIWA SONGEA

Tarehe ya kuwekwa: January 14th, 2018

MAMLAKA ya Udhibiti wa Chakula na Dawa(TFDA) chini ya Idara ya Afya na Ustawi wa Jamii katika Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma imeyafungia maduka ya dawa muhimu 48 kutokana na kushindwa kukidhi vigezo vya uendeshaji wa maduka hayo.

Mganga Mkuu wa Manispaa ya Songea Dk.Mameritha Basike amesema Idara ya Afya imefanyakazi ya utambuzi wa maduka ya dawa muhimu ili kubaini iwapo maduka hayo yanakidhi vigezo kulingana na mwongozo wa uendeshaji wa maduka ya dawa muhimu nchini.

Amesema kati ya maduka hayo yaliyofungiwa, maduka sita yamegundulika yanaendeshwa bila kibali na maduka 12 hayafanyikazi kwa zaidi ya mwaka mmoja licha ya kuwa na vibali vya kuendesha ya dawa muhimu.

Kwa mujibu wa Dk.Basike,katika operesheni hiyo wameaini maduka nane hayajahuisha vibali vya dawa muhimu kwa zaidi ya mwaka mmoja na maduka 22 yamefunguliwa katikati ya mji wa Songea kinyume cha muongozo ya maduka ya dawa muhimu.

Hata hivyo amesema imebainika maduka 23 bado hayajapata kibali cha Mfamasia isipokuwa yana barua iliyotolewa na Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea ya kuruhusiwa kuendesha biashara ya duka la dawa muhimu.

“Kati ya maduka ya dawa muhimu 222  yaliopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea,ni maduka 146  ndiyo yana vibali vya kuendeshea biashara ya maduka ya dawa muhimu’’,anasema Dk.Basike.

Ameongeza kuwa katika operesheni ya utambuzi huo, maduka manne  yamefungwa kwa sababu wamiliki wake wamefariki,wamiliki 11 wamiliki wake wamepewa muda wa miezi sita wa maduka yao kupandishwa hadhi kuwa maduka ya dawa moto(famasi) kwa kuwa maduka yao yalifunguliwa mwaka 2003 kabla ya sheria ya TFDA ya mwaka 2003.

Manispaa ya Songea imefanya utambuzi huo ili kutekeleza agizo la Katibu Mkuu  Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) ya kuyatambua maduka ya dawa muhimu na rejareja yaliyosajiriwa chini ya Baraza la Famasia yanayoendeshwa kisheria.

Katika agizo hilo Katibu Mkuu ameagiza kuyaondoa kwa kuyafunga mara moja maduka yote ya dawa muhimu katika maeneo ya miji mikubwa yalioanzishwa kinyume cha sheria.

Imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI RUVUMA

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

YALIYOJIRI MAKABIDHIANO YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa