• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MAFUNZO YA KUTOA AJIRA ZA MUDA "TASAF" KUTOLEWA MANISPAA YA SONGEA

Tarehe ya kuwekwa: March 2nd, 2022

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

02 MACHI 2022.

Halmashauri ya Manispaa ya Songea ina jumla ya idadi ya walengwa wanaopokea ruzuku ya kaya maskini 5,694, ikiwa miongoni mwa kaya hizo ni 2,625 ambazo zinalipwa fedha taslimu, kaya 2076 zinalipwa kwa mtandao na kaya 993 zinalipwa kwa OTC ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mpango wa kunusuru kaya maskini (TASAF).

Hayo yamebainishwa na Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Christopher Ngonyani ambaye pia ni Mratibu wa TASAF Manispaa ya Songea wakati akifungua mafunzo kwa wawezeshaji wa mamlaka za maeneo ya utekelezaji na usimamizi wa miradi ya kutoa ajira za muda chini ya mpango wa kunusuru kaya maskini – TASAF kwa awamu ya tatu kipindi cha pili yanayofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea leo tarehe 02 Machi 2022.

Alisema kuwa mafunzo hayo yamelenga katika kujenga uelewa kwa wawezeshaji juu ya namna ya kushirikiana na kuwasaidia wananchi kuibua miradi yenye tija ambayo itasaidia kuongeza kipato kwa walengwa hao.

Amewataka wawezeshaji hao kushiriki ipasavyo katika mafunzo hayo kwa muda maalumu uliopangwa,  ambayo yanatarajiwa kufanyika kwa muda wa siku 6.

Akitolea ufafanuzi kuhusiana na mafunzo hayo, Afisa miradi ajira za muda TASAF, Abel Bimbiga alisema kuwa lengo la miradi hiyo ni kutoa fursa za ajira kwa kaya maskini, kutoa ujuzi kwa walengwa itakayowasaidia katika shughuli mbalimbali za maendeleo pamoja na kuwawezesha kupata miundo mbinu ambayo itatoa manufaa katika maeneo husika.

Aliongeza kuwa, mzunguko wa kwanza wa utekelezaji miradi hiyo ulifanyika katika Halmashauri 51 ikiwemo na Halamshauri ya Madaba, Songea vijijini pamoja na Tunduru ambapo katika mzunguko wa pili mradi utafikia Halmashauri 72 ikiwemo na Halmashauri ya Manispaa ya Songea.

“Aidha, Utaratibu wa kutoa mafunzo kwa wawezeshaji utasaidia katika usimamizi wa utekelezaji wa miradi hiyo ambapo zoezi la kuibua miradi litaanza ifikapo Aprili 2022 na utekelezaji wa miradi hiyo utaanzia mwezi Julai katika kipindi cha miezi 6” Bimbiga alibainisha.

Alisema kuwa miradi ya kutoa ajira za muda inalenga kutoa ajira kwa kaya maskini wakati wa kipindi cha hari ili wanakaya hao waweze kupokea ujira utakaowasaidia kuongeza kipato na hivyo kupunguza umaskini katika jamii.

Bimbiga alieleza kuwa katika kipindi cha kwanza cha mpango wa kunusuru kaya za walengwa jumla ya miradi 9,440 ya kutoa ajira za muda ilitekelezwa katika maeneo ya utekelezaji 44 kwa gharama ya shilingi bilioni 119 ambapo kati ya fedha hizo bilioni 83.3 ilitumika kwa ajili ya kulipa ujira kwa walengwa na shilingi bilioni 35.7 zilitumika kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya miradi na usimamizi.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa