• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MAFUNZO YA MFUMO WA FFARS KUTOLEWA KWA MAAFISA WATENDAJI WA KATA NA MITAA.

Tarehe ya kuwekwa: September 21st, 2022

FFARS ( Facility Financial Account and  Report System )   ni Mfumo wa Uhasibu  na Utoaji  taarifa za Fedha kwa ngazi ya kituo cha kutolea huduma, ambao  unasaidia  kuleta  Uwazi na Uwajibikaji na unawezesha utoaji wa  taarifa za mapokezi ya fedha, matumizi, na malipo mbalimbali yaliyofanyika  kwa kuzingatia sheria na taratibu za manunuzi.

Mfumo wa FFARS unasaidia kufahamu kiasi cha fedha  kilichopokelewa, chanzo cha fedha na namna fedha hizo zitakavyotumika katika kufikia lengo lililowekwa la mradi husika ambao unajikita  katika utunzaji  wa vyanzo vya fedha, kwa kutoa taarifa sahihi  ya fedha zote zinazoingia na zinavyotumika.

Mfumo wa FFARS unasaidia kuweka mazingira mazuri kwa wananchi kwa kuwajengea  Imani kwa taasis na Serikali yao kwakuwa inawezesha kufanikiwa kwa kutoa maamuzi sahihi ya matumizi ya fedha za miradi inayotekelezwa ngazi ya jamii.

Katika kufanikisha utekelezaji na usimamizi wa miradi ya maendeleo ngazi ya  kata, na Mitaa, Halmashauri ya Manispaa ya Songea inaendelea  kutoa  mafunzo ya matumizi ya Mfumo wa FFARS kwa Maafisa watendaji wa Kata na Mitaa yanayofanyika kwa muda wa siku 2 kuanzia tarehe 21/09 – 22/09/2022  katika ukumbi wa Manispaa ya Songea  yanayoendeshwa na  wataalam wa TEHAMA.


Afisa TEHAMA Manispaa ya Songea Mvano Mbalale amewataka Maafisa Watendaji wa Mitaa na Kata  kutumia Mfumo wa FFARS ambao unasaidia kutoa picha kamili ya kiasi cha fedha kilichopokelewa na unahakikisha kuwa fedha zinadhibitiwa  vyema sambamba matumizi sahihi yaliyokusudiwa katika mradi  husika.

 Aliongeza kuwa Mfumo wa FFARS  umetengenezwa ili kusaidia kutoa majibu  sahihi ya mahitaji ya fedha kupitia Mfumo  ulioboreshwa katika taasisi au watoa huduma ambao wamekuwa wakitumia mifumo hiyo ambayo imekuwa muhimu katika kutekeleza miradi ngazi ya jamii  tofauti  na mfumo uliokuwa ukitumika  hapo awali

Washiriki wa mafunzo hayo wamesema kuwa wanaipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassani kwa kuwajengea uwezo wa matumizi sahihi ya Mfumo wa uhasibu na utoaji wa taarifa za fedha  FFARS ambao utawasaidia kufanya kazi kwa weredi  mkubwa na kuondoa  mianya ya Rushwa katika mazingira ya kazi. “Walipongeza”

Imeandaliwa na

AMINA PILLY


Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI RUVUMA

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

YALIYOJIRI MAKABIDHIANO YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa