• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mafunzo ya uandaaji wa Mpango na Bajeti kutolewa kwa wakuu wa Idara Manispaa ya Songea.

Tarehe ya kuwekwa: November 18th, 2020

Mwongozo wa Mpango na Bajeti ni nyenzo ya kuandaa na kutekeleza Bajeti ya Serikali na taasisi zake pamoja na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka mmoja mmoja, ambao unatoa maelekezo mahsusi kwa maafisa masuuli juu ya ukusanyaji wa mapato na usimamizi mzuri wa matumizi ya fedha za umma ambao  unatoa ukomo wa Bajeti ya Serikali kwa kuzingatia maoteo ya vyanzo vyote vya mapato ya ndani na nje.

Hayo yametamkwa na Mchumi wa Manispaa ya Songea  Andambike B. Kyomo wakati wa kutoa mafunzo kwa Wakuu wa Idara na vitengo  kwa lengo la kuwajengea uelewa wataalamu hao namna ya  uandaaji wa mpango na bajeti wa Serikali kwa mwaka wa fedha 2020/2021 na 2021/2022  yanayoendeshwa na ofisi ya Mchumi wa Manispaa ambayo yataendelea kutolewa kwa muda wa siku tatu kuanzia  leo 18 hadi 20 novemba 2020,  katika ukumbi wa SACCOS ya Watumishi wa Manispaa ya Songea.

Kyomo alisema”  Mpango ni mchakato wa pamoja wa uandaaji taarifa wenye dira na  lengo linalokusudiwa katika kiwango Fulani na bajeti nimakadirio ya mapato na matumizi ya fedha, ili kuhakikisha mpango unafanikiwa kwa wakati uliotarajiwa.”

Madhumuni ya Mwongozo wa Mpango na Bajeti wa mwaka  ni pamoja na Kuhakikisha       ufanisi katika utayarishaji wa Mipango na Bajeti, Kuainisha vipaumbele vya Serikali vitakavyozingatiwa katika bajeti, pamoja na  Kutoa maelekezo mahususi ya Serikali kwa Maafisa Masuuli watakayopaswa kuyafuata kwenye Mipango na Bajeti za mafungu yao. Kyomo alibainisha.

Aliongeza kuwa kila mpango na Bajeti wa Serikali lazima uzingatie vipaumbele muhimu      vinavyogusa jamii ikiwemo  Kukuza Uchumi na Maendeleo ya Viwanda, Kusimamia na kuendeleza Mipango Miji na Makazi, Maendeleo ya Watu ambayo ni  hatua za kimkakati katika maendeleo ya watu zinazolenga kuboresha   mifumo ya  upatikanaji wa huduma za jamii kama elimu, Afya na Ustawi wa Jamii, Maji Safi na Salama, Majitaka, pamoja na uwezeshaji Wananchi Kiuchumi pamoja  na miundombinu.

Mwisho,  aliwaasa Wataalamu hao kusoma Ilani ya  Chama Cha Mapinduzi mara kwa mara ili wanapoandaa mpango na bajeti wa mwaka husika  lazima uendane na ilani ya Chama Cha  Mapinduzi kujua  nini  kimeelekeza. “Alisisitiza “

IMETAYARISHWA NA;                      

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

18.11.2020

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa