• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MAGARI matano ya Marekani yatakavyosaidia kudhibiti UKIMWI Kusini

Tarehe ya kuwekwa: August 26th, 2018

SERIKALI ya Watu wa Marekani  imenunua magari sita yenye thamani ya Dola za Marekani 192,000 kwa ajili ya kutekeleza Mradi wa Mwitikio wa Kudhibiti UKIMWI katika mikoa mitano ya Nyanda za Juu Kusini ambayo ni Ruvuma,Mbeya,Katavi,Songwe na Rukwa.

Hafla ya kukabidhi magari hayo toka Serikali ya Marekani imefanyika katika viwanja vya bustani ya Manispaa ya Songea,mgeni rasmi akiwa ni Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera,Bunge,Kazi,Vjana,Ajira na Wenyeulemavu Jenista Mhagama.

Wengine waliohudhuria hafla hiyo ni Kaimu Balozi wa Marekani Dkt.Inmi Patterson,Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) Dkt.Leonard Maboko,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme na waratibu wa kuthibiti UKIMWI wa mikoa mitano.

Akizungumza kabla ya kukabidhi magari hayo,Kaimu Balozi wa Marekani Dkt.Inmi Patterson amesema kati ya magari sita yalionunuliwa magari matano yanapelekwa katika mikoa mitano na gari moja linabaki  makao makuu ya TACAIDS kwa ajili ya ufuatiliaji na usimamizi.

Naye Mgeni rasmi katika hafla hiyo,Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Kazi,Vijana ,Ajira na Wenyeulemavu Jenista Mhagama akizungumza kabla ya kukabidhi magari hayo kwa waratibu wa kudhibiti UKIMWI katika mikoa mikoa mitano,ambayo wanatekeleza mradi katika maeneo ya kinga,matunzo,matibabu na kupunguza athari zinazotokana na UKIMWI amewaagiza kuhakikisha wanafanyakazi kwa tija na ufanisi wa hali ya juu.

Ugonjwa wa UKIMWI umekuwepo Tanzania kwa takribani sasa Zaidi ya miaka 30,kulingana na utafiti mikoa mitano ya Nyanda za Juu Kusini imekuwa na viwango vya maambukizi vya juu ya wastani wa viwango vya kitaifa ambao ni asilimia 4.7.

Katika utafiti wa mwaka 2016/2017 wa viashiria vya maambukizi ya virusi vya UKIMWI,takwimu zinaonesha kuwa Mkoa wa Mbeya maambukizi ni asilimia  9.3,Katavi asilimia 5.9,Rukwa asilimia 4.4,Ruvuma ni asilimia 5.6 na Mkoa wa  Songwe ni 5.8,Kutokana na takwimu hizo.ni wazi kuna umuhimu wa uwepo wa mradi wa usimamizi na ufuatiliaji wa muitikio katika ngazi za vijiji,mitaa na kata katika mikoa hiyo mitano ya Nyanda za Juu Kusini ambayo maambukizi yanazidi wastani wa kitaifa ambao ni asilimia 4.7.


Mwandishi ni Albano Midelo

Afisa Habari wa Manispaa ya Songea

Mawasiliano yake ni albano.midelo@gmail.com,simu 0784765917



Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa