• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MAMA ASKOFU GILDA SILUIMBA AMEWATAKA WANAWAKE WA MANISPAA YA SONGEA KUJITAMBUA KATIKA NAFASI ZAO.

Tarehe ya kuwekwa: March 2nd, 2021

“MWANAMKE KATIKA UONGOZI CHACHU KUFIKIA DUNIA YENYE USAWA”

Ni kauli mbiu yenye ukweli usiopingika hapo awali   wanawake hawakuhamasika na kushika nafasi za uongozi katika miaka 1990, wanawake katika kaya walikuwa wanafanya kazi nyingi, ujira kidogo, na unyanyasaji uliokithiri, wanawake kutopewa kipaumbele  kulinganishwa na wanaume.

Hayo yalibainishwa katika  uzinduzi wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 01 machi 2021  iliyofanyika katika uwanja wa Majimaji Manispaa ya Songea  kuelekea siku ya kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani ambayo huadhimishwa kila mwaka ifikapo 08 machi ambapo kimkoa yatafanyika Wilayani Tunduru.

Mgeni rasmi katika uzinduzi wa  maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani Mama Askofu wa Kanisa la REDEEMED  Songea  Mjini Gilda Simon Siluimba ambaye alisema “ Kauli mbiu hii imeandikwa kwa maana ya pekee inawezekana alikuta wanawake ambao bado  hawajitambui  kama wao ni akina nani,” hivyo alichukua nafasi hiyo kuwaeleza wanawake kuwa nilazima mwanamke ujitambue, ujiamini, alafu uone unaweza”.

Mama Askofu Siluimba alisema Kauli mbiu hiyo inakutambulisha wewe  mwanamke ambaye pengine umekata tamaa na kujiona pengine huwezi kufanya jambo lolote, kupitia maadhimisho haya ni  lazima tutambue kuwa  mwanamke chachu inaamanisha kuwa  popote alipo mwanamke mwenye kujitambua  lazima jambo liende vizuri, lazima shughuli zisogee na  kwa ufanisi mkubwa, pia  lazima jambo litaeleweka.

Alisema Tunaishukuru Serikali yetu  kwa kutambua nafasi ya  mwanamke katika jamii haijalishi kipindi cha nyuma  mwanamke hakushiriki kwa usawa kama ilivyo sasa kutokana na Serikali yetu  kutambua nafasi ya mwanamke katika jamii  imesaidia  kwa kiasi kikubwa wanawake hao  kupata nafasi za uongozi mbalimbali katika jamii, kushiriki katika maendeleo, pamoja na fursa ya mikopo kupitia vikundi vya wanawake, mikopo  inayotolewa na Serikali kupitia Maendeleo ya jamii.

Akinukuu Vitabu vya mungu /Maandiko yasemayo “ Alianza kuumbwa mwanaume au kwa namna nyingine tunasema mwanaume ni TOLEO LA KWANZA na mwanamke TOLEO LA PILI, kwasababu maandiko hayo yameeleza bayana kuwa alitolewa ubavuni mwa mwanaume ili kufanywa  kuwa mwanamke kwa hiyo mwanamke ni toleo la pili na kubarikiwa kupewa uwezo mkubwa wa ufahamu wa kufanya mambo mengi kwa wakati, utaalamu mwingi, na akili nyingi na ni nguzo katika familia.” 

Amewataka wanawake wote kuishi kwa kujitambua kwani mwanamke chachu katika familia, chachu katika Serikali, chachu katika Ofisi, Chachu kwenye jamii, chachu katika maendeleo, hivyo ni ukweli usiopingika kuwa  wanamke ni chachu na  ili uwe chachu lazima ujitambue.

Akitoa angalizo kwa wanawake ambao bado hawajitambui kuwa  yawezekana ukaitwa chachu kumbe mwenyewe hujitambui na ukawa bado  unaishi kama TOLEO LA KWANZA.

Naye Mratibu wa Maadhisho ya  siku ya wanawake Duniani Joyce  Mwanja alisema lengo la maadhimisho hayo ni kutoa fursa ya kuelimisha jamii hasa wanawake kuhusu jitihada mbalimbali zinazofanywa na Serikali, Asasi za Kiraia, Sekta binafsi na wadau wengine katika kukuza hali ya wanawake wa kitanzania pamoja na kupata fursa ya kubainisha upungufu na mbinu za utatuzi wa changamoto zinazowakabili wananwake.

Mwanja alisema Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Afya, Wazee, Jinsia na watoto inayotukumbusha  kuendelea kujitambua katika nafasi zao  na  kuendeleza jamii. Alisema Wanawake wa Manispaa ya Songea wanatoa shukrani kwa Serikali ya awamu ya tano kwa kuongeza nguvu ya kuwajengea uwezo wanawake kwa kuendeleza jitihada na kuwawezesha wanawake kiuchumi  kupitia mfuko wa wanawake, vijana na walemavu ambapo katika kipindi cha mwaka 2020/2021 julai hadi disemba Manispaa ya Songea imekopesha jumla ya Tsh 108,669,444.80 ambazo ziligawiwa kwa vikundi vya wanawake, vijana, na walemavu.

Kilele cha maadhimisho hayo kitafanyika Kimkoa Wilayani Tunduru mnamo 08 machi 2021.

KAULI MBIU; “WANAWAKE KATIKA UONGOZI CHACHU KUFIKIA DUNIA YENYE USAWA”

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

01 machi 2021

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bil. 22.9 Kujenga Masoko ya Kisasa Manzese A na B, na Kiwanda cha Kuchakata Mazao ya Nafaka Lilambo

    July 06, 2025
  • MBUNGE SONGEA MJINI AKABIDHI KOMPYUTA NA KUFADHILI UKARABATI WA OFISI ZA POLISI

    June 27, 2025
  • DC Songea bAzindua Dawati la Huduma za Ustawi wa Jamii Stendi ya Mabasi Songea

    June 24, 2025
  • Meya Mbano; Amewataka Wananchi Kulinda Haki za Watoto

    June 16, 2025
  • Tazama zote

Video

Makabidhiano ya Mkataba Soko la Manzese A&B
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa