• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MANISPAA ya Songea ina watu zaidi ya 2000 wasiojua KKK

Tarehe ya kuwekwa: October 15th, 2018

Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma ina Watu Wazima 2,458 wasiojua kusoma,kuandika na kuhesabu(KKK).Afisa Elimu ya Watu Wazima Faraja Yonas amesema  kati yao Wanaume ni 661 na Wanawake ni 1,797.  

 Kwa mujibu wa takwimu za usajili za mwezi Januari hadi Machi,Manispaa ya Songea ina jumla ya Watu Wazima 119,328,Kati yao wanaume ni 58,049 na Wanawake ni 61,279.Yonas amesisitiza kuwa Manispaa ya Songea imejipanga vizuri katika harakati za kuhakikisha watu wazima wote wanajua kusoma, kuhesabu na kuandika Kwa asilimia 100.  

 Anaitaja mikakati ambayo Manispaa ya Songea inachukua kutekeleza lengo la  Elimu ya Watu Wazima kuwa ni kutoa elimu kwa Watu Wazima ili kuwapatia stadi za kazi muhimu kwa ajili ya

 Mikakati mingine ni kuongeza ujuzi wa uzalishaji mali na kuyafahamu mazingira yao Kiuchumi, Kijamii na Kisiasa ili kuyakabili  vema mazingira yao ili kufikia lengo kuu la Elimu ya Watu Wazima.

 Akizungumzia kuhusu kisomo chenye manufaa na  kisomo cha kujiendeleza na uzalishaji mali katika Manispaa hiyo,Yonas amesema Manispaa ina vituo 108 vya MUKEJA vyenye washiriki 2,600, wakiwemo Wanaume 937 na Wanawake 1,663.  

 MUKEJA ni Mpango wa uwiano kati ya Elimu ya Watu Wazima na Jamii.  Katika mpango huu washiriki hujifunza mambo yanayohusu uchumi, na maendeleo ya jamii kwa ujumla, ikiwa ni pamoja na kusoma, kuandika na kuhesabu.  

 Katika mfumo huo Washiriki wenyewe ndiyo wanaopanga jambo la kujifunza, muda muafaka wa kujifunza, na namna ya kujifunza. Kwa maana nyingine mukeja ni Mtaala unaozingatia matakwa ya mwanakisomo katika kujifunza.

 Akizungumzia kuhusu Mpango wa Elimu ya Msingi kwa Watoto Waliokosa(MEMKWA),amesema mpango huo unalenga kuwapatia Elimu watoto  walioikosa Elimu ya Msingi ambao wengi wao wanatoka katika mazingira magumu au familia zenye kipato duni.  

 Manispaa ya Songea ina vituo tisa vya MEMKWA, vyenye jumla ya wanafunzi 103 kati yao Wavulana  50 na wasichana 53.

 Kulingana na Afisa Elimu ya Watu Wazima Manispaa hiyo ina jumla ya wana kisomo 154 wanaohudhuria ambapo hivi sasa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Cuba zina mpango wa kutoa Elimu ya Watu Wazima kwa kutumia Redio, Video, na Televisheni.

Imetolewa na Albano Midelo simu 0784765917

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa