• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MANISPAA ya Songea ina ziada ya chakula tani 40,391.78

Tarehe ya kuwekwa: August 24th, 2018

HALI ya upatikanaji wa chakula katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma ni nzuri ambapo jumla ya hekta 24,340.8 zililimwa msimu wa 2016/2017 na kuzalisha tani 98,671.76. wakati mahitaji ya chakula ni tani 58,280 hivyo kufanya kuwa na ziada ya tani 40,391.76 sawa na asilimia 69.3

Mkurugenzi wa Halmashauri ya  Manispaa ya songea Tina Sekambo amesema Manispaa hiyo  inazalisha zao la Kahawa kama zao kuu la biashara ambapo manispaa imeweka mpango wa kuotesha miche ya kahawa 143,384 katika vitalu sita kwa msimu wa 2018/2019.

" Miche 121,784 inatarajiwa kupandwa katika ukubwa Hekta 72.94 na wakulima 290 watanufaika.Hali hii itasaidia kuboresha na kuinua kipato cha wananchi katika kaya zao'',amesisitiza Sekambo.   

 Ameyataja mazao mengine ya biashara yaliyozalishwa katika msimu wa 2016/2017 ni; Alizeti tani 182, Ufuta tani 32.5, karanga tani 50.7, Soya tani 134.56 na Mbaazi tani 46.4 na kwamba Msimu wa 2016/2017 wakulima walitumia pembejeo kiasi cha tani 19,450 za mbolea, kati ya hizo mbolea tani 173.8 zilikuwa ni za ruzuku ya Serikali. 

Hata hivyo amesema Pembejeo hizo zilitumika Katika mazao ya mahindi, kahawa na mpunga ambapo  Halmashauri ina maduka ya pembejeo za kilimo 45 na  kampuni tano ya pembejeo.Amesema  hali ya zana za kilimo za kisasa katika  Halmashauri imeendelea kuboreshwa kwa wakulima mmoja mmoja na kwenye vikundi kwa kununua na kukopa matrekta 143 madogo na makubwa ambayo yanatumika kuongeza tija katika kilimo.

Akizungumzia kuhusu kilimo cha umwagiliaji,Mkurugenzi huyo amelitaja  eneo linalofaa kwa kilimo cha umwagiliaji kuwa ni la ukubwa wa hekta.2,000,kati ya hizo hekta 195 ndio zinalimwa sawa na asilimia 9.7. na kwamba hadi  sasa kuna skimu tatu za umwagiliaji ambazo miundo mbinu yake imejengwa na zinafanya uzalishaji wa tani 375 za mpunga na tani 113 za viazi vitamu.

Imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Agosti 24,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa