• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MANISPAA ya Songea inavyokabiliana na udumavu nchini

Tarehe ya kuwekwa: October 3rd, 2019

MKOA wa Ruvuma unatajwa kuwa miongoni mwa mikoa mitano nchini ambayo inaongoza kwa utapiamlo na udumavu nchini.

Takwimu za Wizara ya Afya  zilizotolewa mwaka 2017/2018 zinaonesha kuwa udumavu katika Mkoa wa Ruvuma ni asilimia 44  licha ya kwamba  Mkoa unaongoza kwa uzalishaji wa mazao ya chakula.

Kufuatia hali hiyo  ipo haja ya kuwa na mikakati ya kujikwamua katika tatizo la udumavu.Moja ya mikakati hiyo ni kuundwa kwa Kamati za lishe katika kila Halmashauri nchini ambazo zinakutana kila baada ya miezi mitatu.

Kamati ya Lishe  ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea ikiongozwa na Mwenyekiti wake Devota Luwungo imebainisha mikakati mbalimbali iliyochukuliwa ili kukamiliana na udumavu ikiwemo kutoa elimu kupitia vyombo vya habari,vipeperushi na mitandao ya kihabari.

Taarifa ya utekelezaji wa shughuli za lishe katika Idara  ya Afya katika kipindi cha Aprili hadi Juni 2019 inaonesha kuwa asilimia nne ya watoto chini ya miaka mitano wana hali duni ya lishe ikilinganishwa na asilimia 5.4  ya kipindi cha Januari hadi Machi 2019.

Kulingana na taarifa hiyo,jumla ya akinamama 7821 walihudhuria kliniki kati ya hao 7758 walipata madini ya chuma sawa na asilimia 99.2 na   akinamama wajawazito 1914 walipata dawa za minyoo kati  1926  waliotakiwa kupata sawa na asilimia 99.4.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo katika kipindi hicho  watoto hai waliozaliwa ni  2873 kati yao watoto 304 walibainika kuzaliwa na uzito pungufu wa  kilo 2.5 sawa na asilimia 10.6.

Utafiti uliofanyika katika mitaa 95 iliyopo ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea ,umebaini kuwa asilimia 86.43 ya kaya zilizopo katika mitaa hiyo zina vyoo bora na asilimia 48.12 ya kaya hizo zina miundombinu ya kunawa mikono nje ya choo na asilimia 87 ya kaya hizo zina maji safi na salama.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Septemba 3,2019

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa