• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MANISPAA YA SONGEA KUANZA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA HATI FUNGANI.

Tarehe ya kuwekwa: January 14th, 2022

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

13.01.2022

Halmashauri ya Manispaa ya Songea yajipanga kuanza kutumia mfumo wa hati fungami kwa lengo la utekelezaji wa miradi ya kimkakati, kiuchumi na kijamii.

Hayo yamebainishwa katika mafunzo yaliyotolewa na viongozi wa soko la hisa kwa watalaamu, viongozi pamoja na wadau mbalimbali hapo jana 13 Januari 2022 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea kwa lengo la kujenga uelewa juu ya matumizi ya hati fungani za Serikali za mitaa nchini Tanzania.

Akizungumza katika mafunzo hayo   mgeni rasmi ambaye alikuwa ni Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma Steven Ndaki alisema kuwa hati fungani za Serikali za mitaa ni dhamana inayohusisha mikopo kwa Halmashauri ambayo itasaidia kupata fedha zitakazotumika katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo, ambayo yatasaidia katika utekelezaji wa muongozo wa uwekezaji ulioandaliwa mwaka 2019 na Mkoa wa Ruvuma kwa Halmashauri zote 8 kwa lengo la kukuza uchumi wa Halmashauri na Mkoa kwa ujumla.

“Muongozo huo wa uwekezaji unaangalia maeneo mbalimbali ikiwemo na uwekezaji katika eneo la kilimo, ujenzi wa miundombinu bora, ufugaji pamoja na kuwekeza katika majengo makubwa ya biashara “Alibainisha.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa soko la Hisa la Dar es salaam Moremi Marwa alisema kuwa lengo la kutoa mafunzo hayo ni utekelezaji wa agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan lililotolewa Oktoba 2021 kwa Wizara ya Fedha na Wizara ya Tamisemi kushirikiana na soko la Hisa kwa lengo la kuwezesha Halmashauri kupata fedha ambazo zitasaidia kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kwenye Halmashauri nchini.

Alisema kuwa soko la Hisa lipo tayari kutoa ushirikiano kwa Halmashauri ya Manispaa ya Songea ili kufanikisha uwekezaji wa miradi mbalimbali kama ilivyobainishwa katika muongozo wa uwekezaji uliotolewa na viongozi wa Mkoa wa Ruvuma.

Akieleza Mkurugenzi wa Biashara katika Soko la Hisa Dar es salaam Ibrahim Mshindo alisema kuwa lengo la mfumo wa hati fungani ni kurahisisha shughuli za uwekezaji kwa Serikali kuu, Taasisi binafsi, wafanyabiashara pamoja na Serikali za mitaa ili kuleta maendeleo kwa kupata mkopo wenye riba nafuu.

Aidha, Afisa biashara wa Manispa ya Songea Furaha Mwangakala alibinisha kuwa Manispaa ya Songea ina fursa nyingi za uwekezaji ikiwemo na maeneo kwa ajili ya viwanda vidogo na vikubwa, kilimo, ufugaji na biashara,

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Dkt. Frederick Sagamiko alisema kuwa Manispaa ya Songea imejipanga kushirikaiana na sekta binafsi na wadau mbalimbali ikiwemo na wafanyabiashara kwa lengo la kuongeza wawekezaji na kufikia malengo ya kutoka kwenye hadhi ya Manispaa na kuwa Jiji.’Alieleza’

Vilevile, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Hamisi Abdallah Ally amelitaka Baraza la Madiwani Manispaa ya Songea kufanyia kazi na kupitisha mpango wa matumizi ya hati fungani za Serikali za Mitaa ndani ya Halmashauri ili kuweza kuleta maendeleo kwa wananchi.

Akifunga mafunzo hayo, Mstahiki Meya Manispaa ya Songea Michael Mbano, kwa niaba ya Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma,   ametoa wito kwa wataalamu kushirikiana na wafanyabiashara pamoja na sekta binafsi ili kuleta maendeleo katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa