• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MANISPAA ya Songea kupima viwanja 250 kwa ajili ya viwanda

Tarehe ya kuwekwa: September 3rd, 2018

HALMASHAURI ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma imejipanga kupima maeneo mbalimbali kwa kupanga matumizi kulingana na mahitaji ya sasa.

Kwa kuanzia Halmashauri imepanga eneo la Kata ya Lilambo kwa matumizi ya viwanda vidogo ,vya kati na vikubwa na kwamba katika eneo hilo pia kuna maeneo ya maegesho,soko,kituo cha mafuta,makazi na biashara.

Upimaji wa eneo hilo umekwaishaanza ambapo hadi kufikia Agosti mwaka huu zaidi ya viwanja 70 vilikuwa vimepimwa kati ya viwanja 250 ambavyo vinatarajiwa kupimwa.

Hata hivyo katika upimaji unaoendelea,viwanja vinapimwa katika maeneo ambayo yamelipwa fidia tu ambapo Halmashauri ya Manispaa ya Songea imelipa zaidi ya shilingi milioni 47 kati ya shilingi milioni 233.84 zinazotakiwa kulipwa katika viwanja vyote ili viweze kupimwa.

Viwanja ambavyo vimepimwa vipo katika hatua ya mahesabu tayari kupelekwa kwa Mkurugenzi wa Upimaji kwa ajili ya usajili ambapo Halmashauri inaendelea na urasimishaji wa maeneo mbalimbali ya Halmashauri kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Halmashauri ya Manispaa ya Songea inaendelea na mpango wake wa kupima viwanja 6000 katika kipindi cha miezi mitatu katika maeneo ya Makambi,Matogoro,Mkwawa,Chemchem,Seedfarm,Kuchile,Making’inda,Miembeni,Mjimwema,Luwawasi,Ruhuwiko na Ruvuma.

Upimaji katika maeneo hayo unaendelea ambapo hadi sasa viwanja zaidi ya 2805 vimekwishapimwa na kwamba Halmashauri imejipanga kufanya zoezi hili liwe endelevu hasa katika maeneo yote yalioiva kama Mitawa,Shule ya Tanga,Subira na Mletele.

Katika Mpango Mkakati huo Halmashauri imelazimika kushirikiana na wananchi kupima kwa sababu Halmashauri haina fedha za kulipa fidia hali inayosababisha kukosa viwanja vyake yenyewe na badala yake kuwapimia wananchi kwa makubaliano ya kulipa shilingi kati ya 80,000 hadi 100,000 kwa kila kiwanja ili kuondoa makazi holela katika Mji wa Songea.

Imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Septemba 3,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa