• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MANISPAA ya Songea kuwa Kitovu cha Utalii katika Mkoa wa Ruvuma

Tarehe ya kuwekwa: September 17th, 2018

HALMASHAURI  ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma ina fursa na vivutio vingi vya utali ambavyo husababisha  matukio mbalimbali ya shughuli za utalii na za kiutamaduni kufanyika kama vile, Tamasha la Kitaifa la kumbukizi la vita vya majimaji linalofanyika kila mwaka kuanzia 25 Februari mpaka tarehe 27 Februari ambayo ni siku ya kilele na ni siku ambayo walinyongwa mashujaa wa vita vya majimaji,

Matamasha mengine ambayo hufanyika kila mwaka katika Manispaa ya Songea ni  tamasha la Majimaji Serebuka linaloendeshwa na NGO’s ya Songea Mississippi shughuli zinazofanyika ni maonesho ya ujasiliamali, mashindano ya ngoma za asili, study tour, mbio za marathoni, mbio za baiskeli, fiesta na maonesho ya mashujaa wa vita vya Kagera.

Halmashauri ya Manispaa ya Songea ina hifadhi moja ya wanyamapori ambayo ni hifadhi ya Ruhira (Ruhira game reserve) inayosimamiwa na Kikosi cha kuzuia ujangili kanda ya kusini (KDU) chini ya Mamlaka ya Kusimamia Wanyamapori Tanzania (TAWA)

 Kazi kubwa ya sekta ya wanyama pori ni kulinda na kuhimiza ulinzi wa wanyama pori ambao ni hazina ya nchi yetu. Vilevile ni jukumu la sekta kulinda na kuendeleza hifadhi ya wanyamapori katika pori la akiba Ruhira, Kulinda mali na maisha ya wananchi kutokana na wanyama wakali na waharibifu, na uhamasishaji, uhifadhi na ulinzi wa wanyamapori katika mitaa inayozunguka pori pamoja na kufanya doria kwa kuzuia ujangili.

 Halmashauri ya Manispaa ya Songea ina jumla  ya misitu ya hifadhi 10, kati ya hiyo misitu mitatu (West Matogoro 1000.5ha, East Matogoro 7457.24ha na South Matogoro 6755.7ha) ni ya Serikali Kuu inasimamiwa na Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) na misitu 7 (Likuyu 722ha, Kwalikucha 33ha,Namanyigu 7.1ha,Chandamali 29ha,Liumbu 66.8ha na Unangwa 20ha, Nangwai 72.9ha)

Halmashauri kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa mazingira imepanda jumla ya miti 925,146 katika Misitu ya hifadhi Matogoro, vyanzo vya maji vya bonde la mto Ruhila na milima ya Kwalikucha-Liwena ilitoa  jumla ya kilogramu 112 za mbegu za miti na viriba kilogramu 200. Aidha halmashauri ina mizinga 1040 ya ufugaji Nyuki inayomilikiwa na vikundi,taasisi na ya watu binafsi. Hali hii inasaidia kuboresha vyanzo vya maji,kuboresha mazao ya misitu na zao la asali ambapo litasaidia kuongeza kipato cha wananchi.

Imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari wa Manispaa ya Songea 

Septemba 17,2018.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa