• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MANISPAA ya Songea yakopesha wajasirimali wadogo milioni 61

Tarehe ya kuwekwa: June 20th, 2019

HALMASHAURI ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma imetoa mkopo wa zaidi ya milioni 61 katika vikundi 48 vya wajasirimali wadogo.

Akisoma taarifa ya utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake,vijana na makundi maalum kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea,Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii,Naftari  Saiyoloi amesema fedha hizo zimetokana na mapato ya ndani ya asilimia kumi.

Amesema fedha zinazokopeshwa ni mapato ya ndani ya shilingi milioni 40 na fedha za marejesho ya mikopo ambazo ni shilingi milioni 21 na kwamba mikopo inatolewa ili kukamilisha utoaji wa mikopo ya robo ya mwaka wa fedha wa 2018/2019.

“Katika mwaka wa fedha wa 2017/2018 jumla ya vikundi vya wanawake 127 vimekopeshwa shilingi milioni 33.9 hivyo kufanya jumla ya fedha zilizokopeshwa kufikia milioni 196’’,alisisitiza  Saiyoloi.

Mgeni rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Mgema amesema serikali imekwishaagiza kuanzia mwaka wa fedha wa 2018/2019 hakutakuwepo tena na tozo ya riba ya asilimia 10 kama ilivyokuwa katika miaka ya nyuma.

“Fedha hizi mnaazimwa  mkazifanyie kazi na baadaye mzirejeshe,fedha hizi ni za kwenu wanawake,vijana na makundi maalum waliopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea,tunapeana kwa zamu’’,alisisitiza

Hata hivyo Mkuu wa Wilaya ameagiza wale wote waliopewa mikopo kuirejesha kwa wakati ili zitumike kuwakopesha wajasirimali wadogo wengine na kufanya biashara yenye tija kwa kuwa na mkopo mkubwa.

Ameitaja azma ya serikali kuwa na mfuko mkubwa wa kukopesha wajasirimali wadogo hali ambayo itasababisha kutokuwa na sababu tena ya kutenga bajeti.

Halmashauri ya Manispaa ya Songea katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2018/2019 imeweza kutoa mikopo kwa wanawake,vijana na makundi maalum kwa asilimia 91.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Juni 20,2019

 

 

 

                                                     

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa