• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MANISPAA ya Songea yapanda miche 6200

Tarehe ya kuwekwa: January 24th, 2020

Manispaa ya Songea yapanda miche ya miti 6200

HALMASHAURI ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma imeadhimisha siku ya upandaji miti kitaifa Januari 24 kwa kupanda miche ya miti 6200 katika chanzo cha maji Namanditi.

Wananchi wa Kata ya Ruhuwiko wakiongozwa na madiwani wa Manispaa ya Songea  walishiriki kupanda miche ya miti ya asili.Mgeni rasmi katika zoezi hilo alikuwa ni Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea Alhaj Abdul Hassan Mshaweji.

Awali akitoa taarifa ya Idara ya Maliasili Katika Manispaa ya Songea,Mkuu wa Idara hiyo Godfrey Luhimbo alizitaja shughuli za kibinadamu kuwa ndiyo chanzo kikuu cha uharibifu wa mazingira ambapo katika Manispaa ya Songea uharibifu aliutaja kuwa unatokana na uvamizi wa misitu ya hifadhi.

Sababu nyingine alizitaja kuwa ni ukataji miti hovyo kwenye vyanzo vya maji na kwenye misitu ya hifadhi kwa lengo la kuzalisha mazao ya misitu kama vile mkaa,nguzo,kuni na mbao na uwindaji wa wanyama

“Kutokana na uharibifu wa mazingira tunakabiliwa na changamoto nyingi zikiwemo kuongezeka kwa joto la dunia,unyeshaji wa mvua usiokuwa na mpangilio,ukame na maradhi mbalimbali yanayomkabili binadamu’’,alisisitiza.

Katika kukabilina na changamoto hizo ameitaja mikakati inayofanywa na Idara ya Maliasili kuwa ni kutoa elimu,kupanda miti kila mwaka katika maeneo mbalimbali na kufanya doria za mara kwa mara ili kudhibiti uharibifu wa misitu.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Naftari Saiyoloi amewaasa wakazi wa Namanditi kuhakikisha miche ya miti iliyopandwa inatunzwa ili iweze kukua na kusaidia kuimarisha vyanzo vya maji ambavyo ni muhimu kwa maendeleo endelevu.

Naye mgeni rasmi Mstahiki Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea Alhaj Abdul Hassan Mshaweji  amewaasa wananchi wa Songea na watanzania kwa ujumla kulinda miti ambayo ni muhimu  ikiwemo dawa.

“Binadamu anaongoza kwa kuharibu misitu,Mwenyezi Mungu amevileta vitu vyote duniani vinatakiwa vitunzwe,ikiwemo mimea ambayo ni muhimu kwa mazingira endelevu’’,alisema Mshaweji.

Ametoa rai kwa wananchi kuendelea kutunza na kuvilinda vyanzo vya maji vilivyopo ili kuepukana na madhara ya uharibifu wa mazingira ikiwemo ukame ambao unaweza kusababisha viumbe hai kushindwa kuishi.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Januari 24,2020

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa