• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MANISPAA ya Songea yatoa mafunzo kwa walimu 50 wanaofundisha wanafunzi wenye mahitaji maalum

Tarehe ya kuwekwa: November 1st, 2019

HALMASHAURI ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma kupitia fedha za kuwajengea uwezo watumishi (ULGSP) imetoa mafunzo kwa walimu 50 wanaofundisha wanafunzi wenye mahitaji maalum katika shule za msingi na sekondari.

Mafunzo hayo ambayo yamefanyika kwa siku moja kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea,yamefunguliwa na mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Mgema.

Akizungumza kabla ya kufungua mafunzo hayo,Mgema amesema kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwa walimu wanaofundisha wanafunzi wenye ulemavu wa aina mbalimbali wakiwemo wanafunzi wasioona,wasiosikia,wenye ulemavu wa akili na wenye ulemavu zaidi ya mmoja ili walimu waweze kutoa elimu kwa ufanisi.

Amesema serikali kwa kutambua uwepo wa wanafunzi wenye mahitaji maalum,imeweka mazingira ya kuhakikisha kwamba wanafunzi wote wanapata elimu sawa,ndiyo maana serikali imeanzishwa vyuo vya elimu maalum.

“Nawapongeza kwa kazi kubwa ambayo mnaifanya,lakini natambua kuwa tuna upungufu mkubwa wa walimu wa elimu maalum ambao wanaweza kuwasaidia vijana wetu wenye mahitaji maalum ’’,alisema Mgema.

Kwa mujibu wa Mgema,mafunzo hayo yatawawezesha walimu ambao hawakupata mafunzo maalum,kuweza kutambua mambo muhimu kama lugha za alama na maandishi ya nukta nundu ili waweze kusaidia kuwafundisha wanafunzi wenye mahitaji maalum.

Kwa upande wake Afisa Elimu maalum katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea Rehema Nyagawa amesema katika Manispaa hiyo kuna jumla ya wanafunzi 405 wenye mahitaji maalum kati yao wavulana 243 na wasichana 162.

Nyagawa amesema Manispaa ya Songea ina jumla ya walimu 52 tu waliosomea kufundisha wanafunzi wenye mahitaji maalum na kwamba kuna walimu 12 ambao wanafundisha wanafunzi wenye mahitaji maalum bila kusomea elimu maalum.

“Manispaa ya Songea ina upungufu wa walimu wenye mahitaji maalum 13,walimu waliopo ni 52,jumla ya walimu 65 wanahitajika,hivyo kutokana na upungufu uliopo,ni vema kutoa mafunzo ya muda mfupi kwa walimu wasiokuwa na mafunzo maalum’’,alisema Nyagawa.

Akizungumza wakati anafunga mafunzo hayo,Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tina Sekambo amewapongeza walimu wanaofundisha watoto wenye mahitaji maalum na kusisitiza kuwa serikali inatambua kazi ngumu wanayoifanya hivyo wasikate tamaa bali waendelee kuchapakazi.

“Kazi mnayoifanya ni ngumu sana ,iwapo mwalimu anayefundisha wanafunzi wasiokuwa na ulemavu anapata tabu,je ninyi wenye ulemavu….hatuna cha kuwalipa,bali anayeweza kuwalipa ni Mwenyezi Mungu pekee’’,anasisitiza Sekambo.

Manispaa ya Songea ina vitengo tisa ambavyo vinafundisha wanafunzi wenye mahitaji maalum na shule moja maalum ya bweni ya Mtakatifu Vincent inayofundisha wanafunzi viziwi.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Novemba Mosi,2019

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa