• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MANISPAA YAANZA KUPULIZIA MAZALIA YA MBU

Tarehe ya kuwekwa: October 29th, 2017

HALMASHAURI ya Manispaa ya Songea imeanza rasmi upuliziaji mazalia ya mbu katika mitaa 95 iliyopo kwenye kata 21 zilizopo katika Halmashauri hiyo.Afisa Afya Mkuu wa Manispaa ya Songea Vitalis Mkomela amesema zoezi la upuliziaji limeanza Oktoba 19 mwaka huu katika mitaa ya kata za Bombambili, Mfaranyaki, Matarawe na Mjini.

Amesema zoezi limefanyika katika mazalio ya wazi ambayo mbu wa malaria hutaga mayai  na kuzalisha mbu wanaoeneza ugonjwa wa malaria.Kwa mujibu wa Afisa Afya huyo hadi sasa jumla ya mazalio ya maji 212 na mabwawa manane yamepuliziwa dawa na kwamba zoezi hilo linafanyika kata hadi kata.Hata hivyo anazitaja changamoto ambazo zimejitokeza hadi sasa ni zoezi hilo Kutokuwa kwenye mpango wa Halmashauri hivyo kukosa fedha za kununua vifaa na kuwalipa wapuliziaji hali ambayo imesababisha zoezi hilo kuanza katika mitaa 49 iliyopo katika  kata kumi kati ya mitaa 95 iliyopo katika kata 21.

Changamoto nyingine anaitaja kuwa ni Kukosekana kwa maafisa afya katika kata nane,ambao ni wataalam  wa zoezi hili katika kata zao.Anaitaja mikakati ambayo inachukuliwa ili kukabiliana na changamoto hizo kuwa ni Kuandaa bajeti  ya upuliziaji na kuingiza katika mpango  wa mwaka 2018/ 2019.Kabla ya kuanza rasmi kwa zoezi la upuliziaji,Halmashauri ya Manispaa ya Songea ilianza kutekeleza zoezi la upuliziaji kwa kufanya mkutano elekezi kwa wenyeviti na Maafisa watendaji  wa mitaa 49 ambayo ipo katika kata kumi.

Mkutano huo ulijadili masuala muhimu ya zoezi la kuua viluwiluwi wa mbu,kuhamasisha wananchi Kutambua mazalio ya mbu katika maeneo yao na namna ya kumteuwa mpuliziaji wa viuadudu wa kujitolea kutoka katika mitaa yao.Baada ya mkutano huo  wenyeviti wa mitaa na maafisa watendaji waliteua mpuliziaji kutoka katika kila mtaa ambao walifanyiwa mafunzo namna ya kupulizia viuadudu katika mazalio ya wazi na mazalio yaliyofunikwa.

Imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa