• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MANISPAA YATOA MILIONI 45 KWA WAJASIRIMALI WADOGO

Tarehe ya kuwekwa: October 16th, 2017

HALMASHAURI ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma imetoa jumla ya sh.milioni 45 kwa ajili ya kutoa mikopo katika vikundi  49 vya wajasirimali wadogo.Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii katika Manispaa hiyo Naftari Saiyoloi ametoa taarifa hiyo katika uzinduzi wa mfuko wa vijana na wanawake kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Amebainisha kuwa sh.milioni tisa zitakopeshwa kwa vikundi kumi vya vijana na sh.milioni 36 zitakopeshwa vikundi 39 vya wanawake.Saiyoloi amebainisha kuwa kuanzia mwaka wa fedha wa 2014/2015 hadi mwaka wa fedha wa 2017/2018 Manispaa ya Songea imetoa zaidi ya sh.milioni 181 kwenye mfuko wa wanawake na vijana.Hata hivyo amesema kati ya fedha hizo,sh.milioni 116 zinatokana na mapato ya ndani na zaidi ya milioni 65 zinatokana na marejesho yaliofanyika kutokana na vikundi vinavyokopeshwa na kurejesha mkopo.

“Idadi ya vikundi vya wanawake vilivyonufaika kwa fedha hizi ni 202 na kiasi kilichokopeshwa ni zaidi ya milioni 126,idadi ya vikundi 115 vya vijana vilinufaika na mkopo wa zaidi milioni 55’’,alisema Saiyoloi.Kwa mujibu wa Afisa Maendeleo huyo,Manispaa ya Songea katika kipindi hicho ilitoa jumla ya sh.milioni 92 kutoka mapato ya ndani kwa ajili ya mfuko wa wanawake na vijana.

Amesema kati ya fedha hizo milioni 3.2 zilitumika kwa ajili ya usimamizi na ufuatiliaji na milioni 88.8 vilikopeshwa vikundi vya wanawake 77 kiasi cha sh.milioni 59.8 na vikundi vya vijana 56 vilikopeshwa milioni 29.Amebainisha kuwa fedha za vikundi vya wanawake zilizorejeshwa ni zaidi ya milioni 53 na fedha za vikundi vya vijana zilizorejeshwa ni zaidi ya milioni tisa.

Mgeni rasmi katika utoaji wa mikopo hiyo,Mbunge wa Jimbo la Songea mjini Leonidas Gama ameipongeza Manispaa ya Songea kwa kutoa kwa wakati asilimia kumi ya mapato ya ndani kwa ajili ya kukopesha vijana na wanawake.Amesema mikopo hiyo ni muhimu kwa wanawake na vijana kwa sababu umasikini mkubwa upo katika ngazi ya familia ambapo mkopo huo unachangia kupunguza umaskini kwa wanyonge.

Taarifa imetolewa na 

Albano Midelo Afisa Habari wa Manispaa ya Songea

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa