• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MASALIO ya mijusi iliyoishi miaka milioni 240 iliyopita yagundulika Ruvuma

Tarehe ya kuwekwa: July 28th, 2018

MASALIO ya aina tatu za mijusi ambayo inaaminika iliishi miaka milioni 240 iliyopita yamegundulika katika Pori la Akiba la Litumbandyosi,Bonde la Ruhuhu wilayani Mbinga mkoani Ruvuma.

Afisa Maliasili na Utalii wa Mkoa wa Ruvuma Afrikanus Challe anasema ugunduzi huo licha kuongeza vivutio vya utalii katika Pori la Akiba la Litumbandyosi,lakini pia unaongeza vivutio vya utalii katika Mkoa wa Ruvuma hali ambayo itafungua milango ya utalii.Masalia ya mabaki ya mijusi hiyo,yamegundulika katika maeneo ya Manda,Lifua,Kingori na Usili ndani ya Bonde la Ruhuhu  na kwamba masalia ya mijusi  inaaminika imeishi miaka mingi zaidi duniani ukilinganisha na aina nyingine za masalia ya mijusi

Ugunduzi wa masalia mengine ya mijusi katika Bonde la Ruhuhu mkoa wa Ruvuma yanafungua milango ya utalii katika ukanda wa kusini wenye mikoa ya Ruvuma,Lindi na Mtwara.Wanasayansi waliogundua,aina tatu za masalia ya mijusi bonde la Ruhuhu wanazitaja aina hizo kuwa ni ruhuhuensis iliyogunduliwa katika eneo la Kingori, ruhuhuaria ambayo imegundulika eneo la Manda Lifua na masalia ya mijusi aina ya ruhuhucerberus eneo la Kawinga.

Mgunduzi wa masalia ya mijusi ya ruhuhuaria anaitwa Fransis Perrington ambaye anaaminika aliyagundua kwa mara ya kwanza mwaka 1930 katika miamba tabaka ya  Lifua Manda Bonde la Ruhuhu.Masalia ya mjusi aina ya Ruhuhucerberus yaligundulika eneo la Kawinga mwaka 2002 na masalia ya awali ya mijusi ya Ruhuhuensis iligundulika mwamba wa Usili Bonde la Ruhuhu mwaka 1950.

Hata hivyo Utafiti wa mwisho kuhusiana na masalia ya mijusi hiyo ulifanyika kati ya mwaka 2007 na 2008 na Timu ya watafiti toka nchi za Uingereza na Marekani na kugundua idadi kubwa ya masalia ya mijusi hiyo katika Bonde la Ruhuhu.

Watafiti hao wa kimataifa wa Makumbusho,wakioongozwa na Ken Angielzyk na Bill Simpson walikuwa ni miongoni mwa wanasayansi wa kimataifa waliofika Bonde la Ruhuhu kufanya uchunguzi na kufanikiwa kukusanya idadi kubwa ya masalia ya mijusi ambayo inaaminika iliishi miaka mingi zaidi duniani.

“Masalia haya ya mijusi jamii ya mamba  yalijadiliwa katika nyaraka (Thesis) kadhaa katika chuo kikuu cha Cambridge,Uingereza,inakadiriwa kwamba jamii hiyo ya mijusi iliishi bonde la Ruhuhu miaka milioni 240 iliyopita’’,anasema Afrikanus Challe Afisa Maliasili na Utalii wa Mkoa wa Ruvuma.

Kulingana na vipimo vya kiikolojia kwenye mabaki ya mijusi hiyo,inaaminika dinosaurs wa Bonde la Ruhuhu ana  urefu wa meta kati ya 2.7 hadi 10,ana shingo ndefu na mkia, na alikuwa na miguu minne kama mamba.

Challe anasema ugunduzi wa masalia ya mijusi katika bonde la Ruhuhu ni mafanikio makubwa kwa wanasayansi hao kwa sababu wamegundua kile wanachoita kama ni chanzo cha  kizazi cha dinosaurs na kwamba ugunduzi huo mpya umejaza pengo kubwa katika historia ya mabaki ya mjusi huyo adimu duniani.

Tanzania imebahatika kuwa na masalia ya viumbe adimu duniani ambavyo vinavutia watalii kila kona hapa nchini kufika kufanya tafiti na kutembelea katika maeneo husika.Moja ya vivutio hivyo ni masalia ya mjusi ambaye anafahamika kwa jina la Tendaguru  anayepamba makumbusho ya Ujerumani ambaye masalia yake yaligundulika mkoani Lindi.

Masalia ya mjusi huyo yalivumbuliwa katika eneo la Tendaguru wilayani Kilwa mkoani Lindi zaidi ya miaka 100 iliyopita.Mjusi huyo ni kuvutio adimu katika Makumbusho ya Berlin nchini Ujerumani ambaye ana uzito wa tani 50.Mjusi huyo anakadiriwa kuwa na umri wa miaka milioni 150,ana urefu wa meta 13.7 kwenda juu,anakadiriwa kuwa na moyo wenye uzito wa kilo 400 na chakula cha mjusi huyo kilikuwa ni m

Mwandishi wa makala haya ni Albano Midelo,mawasiliano albano.midelo@gmail.com,simu 0784675917


Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBUNGE SONGEA MJINI AKABIDHI KOMPYUTA NA KUFADHILI UKARABATI WA OFISI ZA POLISI

    June 27, 2025
  • DC Songea bAzindua Dawati la Huduma za Ustawi wa Jamii Stendi ya Mabasi Songea

    June 24, 2025
  • Meya Mbano; Amewataka Wananchi Kulinda Haki za Watoto

    June 16, 2025
  • Meya wa Songea Atoa Wito kwa Familia Kuchangia Damu Kuokoa Maisha.

    June 14, 2025
  • Tazama zote

Video

Mbunge Akabidhi Kompyuta 6 na Kufadhili Ukarabati wa Ofisi za Polisi
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa