• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MATUMIZI ya mkaa ni gharama,tumia nishati mbadala

Tarehe ya kuwekwa: June 3rd, 2018

TUKIWA katika maadhimisho ya wiki ya mazingira duniani ambayo inaanza Mei 31 na kilele chake Juni 5 kila mwaka,kauli mbiu ya mwaka huu inasema matumizi ya mkaa ni gharama,tutumie njia mbadala.

Katika tafiti zilizofanywa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Makazi (UN HABITAT) mwaka 2008 zimeonesha kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi zinaongoza kwa matumizi ya nishati ya mkaa.

Utafiti wa kimataifa unaonesha kuwa watu bilioni tatu duniani kati ya bilioni saba wanatumia mkaa na kuni kwa ajili ya kupikia na shughuli nyingine zinazohitaji nishati ya mkaa na kuni hali ambayo inaiweka Dunia njia panda katika suala la kuzuia uteketezaji wa misitu.

Hii ina maana ya kwamba uharibifu wa mazingira hasa ukataji wa miti holela ni mkubwa na unahitaji nguvu ya ziada kwa wadau kutoka ngazi zote kuanzia familia,Kitongoji,Mtaa Kijiji,Kata,Tarafa,Wilaya ,Mkoa,Taifa na kimataifa  kwa ujumla ili kurekebisha na kurudisha miti inayokatwa kwa ajili ya uchomaji mkaa na kuni.

Mabadiliko ya tabianchi ambayo yanaendelea kutokea katika maeneo mbalimbali nchini na duniani kote kwa ujumla ni dalili kuwa binadamu wamefanya uharibifu mkubwa wa mazingira yanayowazunguka hasa vitendo vya ukataji wa miti hovyo.

Takwimu zinaonesha kuwaTanzania inapoteza kiasi cha hekta 400,000 za misitu kila mwaka kwa sababu ya ukataji miti unaochochewa na matumizi ya kuni, mkaa, mbao, ujenzi ama uchomaji moto misitu.Matumizi ya mkaa mijini ni makubwa kuliko vijijini wakati matumizi ya kuni vijijini ni makubwa kuliko mijini.

Waziri Mstaafu wa  Maliasili na Utalii Prof.Jumanne Maghembe anasisitiza kuwa  moja ya vitu ambavyo vinaongoza kwa kuteketeza misitu ni biashara ya mkaa  ambapo anashauri mikoa michache ambayo hakuna ukataji mkaa wa kutisha kama Mkoa wa Ruvuma,waanze kutumia sheria ndogo ndogo ili kukabiliana na watu wanaofanyabiashara hiyo ambayo imesababisha asilimia 60 ya Tanzania kuathirika na jangwa.

”Nani amemuona mtu anayekata miti na kufanya biashara ya mkaa amekuwa tajiri,utamuona ana majivu tu kila siku, kwa sababu miti hii ni viumbe hai  na wanaoikata wanafanya dhambi kubwa sana kwa Mwenyezi Mungu’’,anasema Prof.Maghembe

Utafiti uliofanywa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (Tanzania Forest Services (TFS) chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Mradi wake wa tathmini ya rasilimali za misitu Nchi unaonesha kuwa ukataji huo wa misitu unasababishwa kuzalishwa kwa zaidi ya tani milioni moja za mkaa kila mwaka ambao nusu yake yaani tani 500,000 unatumiwa na wakazi wa Jiji la Dar es Salaam pekee.

Dk. Felician Kilahama ni Mkurugenzi Mstaafu, Idara ya Misitu na Nyuki katika Wizara ya Maliasili na Utalii  anasema  teknolojia inayotumika kutengeneza mkaa  inasababisha kupatikana mkaa kidogo wakati miti mingi imetumika. Kwa mfano, mtegeneza mkaa kwa kutumia tanuru la udongo hupata tani moja ya mkaa kwa kutumia tani 10 hadi 12 za miti iliyokatwa.

Dk.Kilahama anaishauri Serikali kutafuta njia mbadala ya kupikia kwa kutumia gesi kama LPG (Liquefied Petroleum Gas) au hata gesi asilia (Natural Gas) pamoja na vyanzo vingine kama kutumia umeme  badala ya mkaa.

Kutokana na misitu tunapata dawa za asili ambapo utafiti unaonesha kuwa asilimia 75 ya dawa za hospitali vyanzo vyake ni misitu ya asili na mimea mbalimbali. Kwa hiyo jitihada zifanyike ili kuinusuru misitu ya asili isiendelee kuangamia kwa mahitaji makubwa ya mkaa.

Makala haya yameandaliwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Juni 3,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa