• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MBUNGE SONGEA MJINI AFADHILI UPIMAJI WA AFYA YA MACHO KWA WANANCHI WAKE.

Tarehe ya kuwekwa: October 15th, 2021

NA,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

15.10.2021

Wananchi wa Manispaa ya Songea wampongeza Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini na Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe Dr. Damas Ndumbaro kwa kufadhili huduma ya upimaji wa afya ya macho bure, zoezi ambalo limeanza kufanyika  leo tarehe 15 hadi 17 Oktoba 2021 katika eneo la bustani ya Manispaa ya Songea kwa lengo la kusheherekea  maadhimisho ya siku ya afya ya macho duniani.

Akizungumza kwa niaba ya Mbunge, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea Michael Mbano amewashukuru wataalamu wa afya ya macho kutoka katika Hospitali ya St. Joseph Peramiho kwa kukubali kufanya zoezi la kutoa elimu juu ya afya ya macho na jinsi ya kutunza na kuzuia upofu wa macho pamoja na uchunguzi wa macho kwa wananchi wote waliopo ndani ya Manispaa ya Songea.

Mbano ametoa wito kwa wananchi wote kutumia fursa hii kwa kujitokeza kwa wingi ili kupima afya ya macho, huduma ambayo inatolewa bure kwa udhamini wa Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini.

Kwa upande wake Katibu wa Mbunge Jimbo la Songea Mjini Joel Alex Ndunguru, amesema lengo la Mbunge kufadhili zoezi la upimaji wa afya ya macho kwa Wananchi ni kutokana na kuwepo kwa changamoto kubwa ya watu wenye matatizo ya macho wanaohitaji msaada kutoka katika ofisi yake na hiyo ikapelekea kuwaomba wataalamu wa afya ya macho kutoka Hospitali ya St Joseph Peramiho kuwapima wananchi wake bure pamoja na kutoa huduma ya dawa na miwani kwa gharama nafuu.

Nae Mtaalamu wa afya ya macho Dr. Goodlove Kyando amesema kuwa zoezi hili ni la muda wa siku tatu kuanzia leo hadi tarehe 17 Oktoba 2021, na hivyo wananchi wajitokeze kwa wingi ili waweze kujua afya ya macho hasa ugonjwa wa presha ya macho ambao hauwezi kujulikana hadi upate vipimo sahihi kutoka kwa wataalamu wa afya ya macho.

Amesema kuwa watoto wamepewa kipaumbele kikubwa katika zoezi hilo ambapo amewasisitiza wazazi na walezi kuwaleta watoto wao ili waweze kupimwa na kupatiwa matibabu bure kabisa ikiwemo dawa, miwani na operesheni pale inapohitajikaa.”Kyando Alisisitiza”

Wananchi na viongozi mbalimbali ikiwemo na Madiwani wa Manispaa ya Songea wamejitokeza kwa wingi katika zoezi hilo la upimaji wa afya ya macho na wamempongeza Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini kwa kufadhili zoezi hilo pamoja na kupongeza huduma nzuri ya upimaji wa macho inayotolewa na wataalamu wa afya ya macho kutoka St Joseph Mission Hospital Peramiho.

Kauli mbiu ya siku ya macho duniani ni; ‘YAPENDE MACHO YAKO, NENDA KAPIME SASA, KILA MTU ANAHUSIKA’

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa