• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MBUNGE WA SONGEA MJINI AZINDUA MKAKATI WA KUBORESHA UFAULU KATIKA SEKTA YA ELIMU MSINGI NA SEKONDARI

Tarehe ya kuwekwa: December 29th, 2021

Na; 

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

29.12.2021

Halmashauri ya Manispaa ya Songea imefanya tahimini ya mkakati wa uboreshaji wa Elimu ya  ufaulu katika sekta ya elimu msingi na sekondari kwa mwaka 2022.

Tathimini hiyo imefanyika leo tarehe 29 Desemba 2021 katika ukumbi wa shule ya wasichana (Songea girls) Manispaa ya Songea na kuhudhuriwa na Waziri wa Maliasili na Utalii (Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini) Dkt. Damas Ndumbaro, Waheshimiwa Madiwani, wakuu wa shule za Msingi na Sekondari, wadau wa elimu pamoja na viongozi mbalimbali kutoka ndani ya Manispaa ya Songea.

Akizungumza katika tathimini hiyo Mgeni rasmi Dkt. Damas Ndumbaro amewataka walimu kuhakikisha wanazingatia miiko ya taaluma yao pamoja na kuhakikisha wanajiendeleza kielimu kwa lengo la kuboresha sekta ya elimu nchini na kutoa elimu bora kwa wanafunzi.

Dkt. Ndumbaro ametoa wito kwa walimu kuzingatia uwepo wa michezo mashuleni kwa kuandaa bonanza mbalimbali kwa lengo la kuimarisha afya ya mwili na akili ya wanafunzi ambapo amehaidi kutoa vifaa vya michezo kwa kwa shule ambazo zitakuwa tayari kushiriki katika matamasha mbalimbali ya michezo.’Alisisitiza’

Amewapongeza walimu wa Manispaa ya Songea kwa kuendelea kufanya vizuri katika matokeo ya mitihani ya darasa la saba, kidato cha nne na kidato cha sita ambapo alitoa zawadi kwa walimu waliofanya vizuri zaidi kwa somo la Hisabati ambapo walimu waliopokea zawadi hizo kutoka shule mbalimbali ikiwemo na shule ya wavulana Songea (Songea Boys), shule ya wasichana Songea (Songea Girls), shule ya Sekondari Matarawe, shule ya Sekondari Msamala, shule ya sekondari Ruvuma pamoja na shule ya sekondari Bombambili,n.k

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Dkt. Frederick Sagamiko   ametoa wito kwa wazazi na walezi kuhakikisha wanachangia mchango wa chakula kwa wanafunzi wanapokuwa shuleni ikiwa ni miongoni mwa mikakati itakayosaidia kuongeza uboreshaji wa ufaulu kwa wanafunzi.

Dkt. Sagamiko aliongeza  kuwa sababu ya kuwepo kwa tathimini ya mpango shirikishi wa elimu ni kuhakikisha mikakati iliyowekwa inafanyika kwa kushirikiana kwa pamoja ili kuleta tija na mabadiliko katika Nyanja ya elimu ndani ya Manispaa ya Songea kwa mwaka 2022.

Amewataka walimu, Maafisa elimu kata pamoja na watendaji kata kuhakikisha wanawajibika katika nafasi zao ili kuweza kutekeleza mikakati iliyowekwa kwa kila mmoja asimame kwenye majukumu aliyopangiwa.

Akibainisha mikakati iliyowekwa ya uboreshaji ufaulu katika sekta ya elimu msingi na sekondari kwa mwaka 2022, Afisa elimu Sekondari Manispaa ya Songea Devotha Luwungo  alisema kuwa lengo kuu la mkakati huo ni kutumia rasilimali watu na fedha ili kufikia ufaulu wa asilimia 98% hadi 100% kwa shule za msingi, ufaulu wa daraja la I hadi III kwa kidato cha nne pamoja na daraja la I hadi II kwa kidato cha sita.

Alisema kuwa ili kufikia kiwango cha ufaulu wa asilimi 98%-100% Manispaa ya Songea imejipanga kuhakikisha muhtasari (syllabus) zinakamilishwa ifikapo mwezi wa 5 kwa shule za msingi na mwezi wa 6 kwa shule za sekondari ili kutoa nafasi ya wanafunzi kufanya marudio pamoja na uboresahji wa mbinu za ufundishaji ikiwemo na ufundishaji kwa njia ya majadiliano, ziara za moasomo pamoja na matumizi ya zana za kufundishia.”Alibainisha”

Akieleza majukumu ya wadau mbalimbali wa elimu Afisa elimu Msingi na Awali Frank Sichalwe alisema kuwa kila mdau wa elimu katika nafasi yake anatakiwa kuhamasisha wazazi kushiriki katika shughuli mbalimbali za maendeleo ikiwemo na kuchangia ujenzi wa miundombinu ya shule pamoja na kuhamasisha jamii kutoa ushirikiano  katika kudhibiti utoro kwa wanafunzi kwa lengo la kuboresha kiwango cha ufaulu mashuleni.

Akisisitiza ushirikiano kati ya walimu na viongozi wa Serikali za mitaa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea Michael Mbano amewataka wakuu wa shule na viongozi wa bodi za shule kuhakikisha wanashirikiana na viongozi wa Serikali za Mitaa pamoja na Madiwani kwa lengo la kutekeleza mikakati iliyowekwa kwa pamoja.

Halmashauri ya Manispaa ya Songea ina jumla ya shule ina jumla  za Msingi 94 ambapo shule 80  ni za Serikali  na 14 ni shule za binafsi zenye idadi ya wanafunzi wa shule za Serikali ni 55,548 ( Wav 27609, Was 27939) na shule binafsi ni 4,1969 (Wav 1,877 na Was 2319).

Kwa upande wa Elimu Sekondari ina jumla ya shule 42, kati ya hizo 24 ni shule za Serikali na 18 ni shule binafsi ambapo hadi kufikia mwezi 2021 katika shule za Serikali ina jumla ya wanafunzi 16817 ikiwa  na wavulana 7919 na wasichana 8900 pia katika shule binafsi zina jumla ya wanafunzi  2823  kwa wavulana 1519 na wasichana 1304.

Wadau walioshiriki kikao hicho, walitoa maoni yao kwa pamoja na walikubali  kupitisha mkakati wa kuboresha elimu ambapo amewataka walimu wote Manispaa ya Songea kupokea na kutekeleza mkakati huo ili uweze kuleta tija katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea.

Mwisho

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa