• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MEYA MBANO AMEZITAKA TAASISI ZOTE KUTOA ELIMU YA MALEZI KWA JAMII ILI KUTOKOMEZA VITENDO VYA UKATILI KWA WATOTO.

Tarehe ya kuwekwa: June 17th, 2022

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

17 JUNI 2022        

Kila mwaka tarehe 16 Juni Tanzania inaungana na nchi zingine za Afrika kuadhimisha siku ya Mtoto wa Afrika.

Chimbuko la maadhimisho haya ni azimio lililopitishwa na Umoja wa nchi huru za Afrika (OAU) mwaka 1990 kwa lengo la kuwakumbuka watoto wa kitongoji cha Soweto nchini Afrika kusini waliouawa tarehe 16 Juni 1976 kutokana na ubaguzi wa rangi.

Katika Manispaa ya Songea Maadhimisho hayo yamefanyika  jana Juni 16, 2022 katika viwanja vya Zimanimoto na kuhudhuriwa na wananchi  mbalimbali, viongozi,  walimu, wadau mbalimbali  pamoja na wanafunzi wa shule za msingi na sekondari zilizopo ndani ya Manispaa ya Songea.

Akizungumza katika maadhimisho hayo Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea Michael Mbano alisema kuwa Serikali itaendelea kuhakikisha watoto wanapata haki zao za msingi hasa kupata  elimu ambapo watoto wataendelea kusoma bure kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha sita kama ilivyoelezwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan.

Amewataka wazazi na walezi kuhakikisha wanazungumza na watoto ili kubaini changamoto mbalimbali wanazokutana nazo hasa vitendo hatarishi wanavyotendewa wanapokuwa nje na maeneo ya nyumbani.

Ametoa rai kwa walimu kuwa na mahusino ya karibu na watoto pamoja na kuwatunza ili kuimarisha ulinzi wa watoto wanapokuwa shuleni.

Mbano amaezitaka Taasisi zisizo za kiserikali zinazohusiana na utetezi wa haki za watoto kuendelea kutoa elimu ya malezi kwa jamii kwa lengo la kutokomeza vitendo vya ukatili kwa watoto ikiwemo na ubakaji, ulawiti pamoja na mimba za utotoni.”Alibainisha”

Alisema watoto wote kutoa taarifa juu ya ukatili unaofanywa na baadhi ya watu wasiona mapenzi mema, ambapo amewarai wanafunzi hao kutoa taarifa mapema kwa walimu, viongozi wa Serikali za mitaa pamoja na dawati la jinsia lililopo katika vituo vyote vya polisi,  mara wanapoona kuna changamoto za zinazoashiria ukatili.

Pia, amewataka watoto kuwa mabalozi kwa jamii kuhusiana na umuhimu wa kushiriki katika zoezi la sensa ya watu na makazi linalotarajiwa kufanyika ifikapo Agosti 23, 2022 nchini Tanzania.

Kwa upande wake Mratibu wa Maadhimisho hayo Joyce Mwanja (Afisa maendeleo ya jamii Manispaa ya Songea) alisema kuwa kauli mbiu ya maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika mwaka huu ni “Tuimarishe ulinzi wa mtoto, tokomeza ukatili dhidi yake, jiandae kuhesabiwa” ambayo inakumbusha jamii juu ya wajibu wa kuimarisha ulinzi kwa watoto pamoja na kupinga vitendo vya kikatili wanavyofanyiwa watoto katika jamii.’Alisisitiza’

Mwanja alisema kuwa Manispaa ya Songea imetumia siku hiyo kwa kutoa elimu juu ya kupinga ukatili wa watoto, chanzo na madhara yake kuanzia ngazi ya shule za msingi hadi sekondari.

Ametoa rai kwa vikundi mbalimbali vya wajasiriamali na vikoba kuweka ajenda ya kujadili malezi ya watoto katika jamii katika vikao vyao ambayo itawawezesha kuwapa elimu watoto juu ya namna ya kugundua mazingira hatarishi na namna ya kujilinda dhidi ya vitendo vya ukatili.

Mwisho.



Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI RUVUMA

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

YALIYOJIRI MAKABIDHIANO YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa