• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MFAHAMU mwanafunzi wa kwanza kitaifa kidato cha sita 2018

Tarehe ya kuwekwa: July 15th, 2018

MWANAFUNZI bora kitaifa katika matokeo ya mitihani ya kidato cha sita iliyofanyika mei mwaka huu, Anthony Mulokozi amesema, juhudi za kujisomea, kuwasikiliza walimu, ushirikiano na wenzake na kumuomba Mungu vimempa ushindi huo.

Kijana huyo aliyekuwa akisoma mchepuo wa PCB katika Sekondari ya Serikali ya Mzumbe iliyopo Morogoro ameyapokea matokeo hayo kwa shangwe kubwa.Antony ana ndoto ya kuwa daktari. Amesema akiwa nyumbani kwao Ngara mkoani Kagera kuwa, alipata taarifa za matokeo kutoka kwa kaka yake aliyemwambia matokeo yametoka, ampe namba yake ya mtihani.

Alisema baada ya kujua matokeo, alifurahi sana na kumshukuru Mungu, na kukimbilia shambani kumpa taarifa mzazi wake ambaye naye, alifurahi na wakaongozana kwenda internet café kuangalia hizo habari na kukuta amepata A zote.Hisia zake “Nilikuwa najua nitafanya vizuri, lakini sikutegemea kama nitakuja kuwa mwanafunzi bora kitaifa, ila nilijua nitafaulu vizuri,” alisema.

Alitaja siri ya mafanikio yake, kwanza ni kumuomba Mungu, kumtanguliza Mungu mbele lakini pia na kusoma sana.“Nilijitahidi kweli kusoma sana kwa kushirikiana na wenzangu, ndio kuna vitu vingine nilikuwa nafahamu na vingine sifahamu nilikuwa nauliza kwa wenzangu”.

Alisema siri nyingine ni kusikiliza walimu, “walimu wa Mzumbe kwa kweli walitutrain (kutufunza) vizuri jinsi ya kujibu maswali na kujiamini katika chumba cha mitihani, nawashukuru sana, lakini nilijitahidi sana kujipa muda wa kusoma, wakati wa likizo nilikuwa narudia pale nilipokuwa nashindwa shuleni, na siku nyingine nilikuwa nasoma zaidi ili walimu wakija kutufundisha nijue ni nini kinaendelea” alisema.

Amesema, alikuwa anafanya mazoezi ya kutosha huku akijitahidi kutafuta mitihani mingine, kuipitia na kuuliza wenzake na walimu. Ilikuwaje chumba cha mitihani?Anasema kwenye chumba cha mtihani alijitahidi sana kumtanguliza Mungu na kutulia: ”panic (hofu) ni mbaya sana, lakini niliamini nikisoma vizuri tu nitapata cha kujibu, kwa hiyo nilikuwa nikiona swali hili nalifahamu nilijitahidi kulijibu vizuri,”.

Pia alisema wazazi wake walijitahidi kumtia moyo, kwamba ajitahidi, ndugu zake pia walimtia moyo tangu mwanzo wakimwambia kwamba masomo ni magumu lakini akisoma vyema atashinda.

Ratiba ya kujisomea"Saa moja hadi saa nane tulikuwa na walimu na kuanzia saa 8:30 tulikuwa tunakwenda kula, halafu saa 9 mpaka saa 11:30, baada ya hapo nakwenda kuoga halafu saa moja nakwenda kipindi cha dini mpaka saa mbili, then prep nilikuwa nakwenda saa 2 mpaka saa 6:30 au saa saba hivi"amesema

CHANZO NI GAZETI LA SERIKALI LA JULAI 14,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa