• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MH. WAZIRI SELEMANI SAID JAFO AIPONGEZA MANISPAA YA SONGEA KWA UTEKELEZAJI BORA WA MIRADI.

Tarehe ya kuwekwa: December 23rd, 2020

Machinjio hii ikikamilika wekeni mifumo mizuri na  salama ya ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri yetu kwasababu, TAMISEMI imeanzisha miradi hii ili Halmashauri zetu ziweze kukusanya mapato.

Kauli hiyo imetemkwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mh. Selemani Said Jafo akiwa katika ziara ya kutembelea  miradi ya miundombinu ya  Barabara, ujenzi wa machinjio Mpya ya kisasa, pamoja na kituo cha stendi cha mabasi Tanga na kisha alifanya mkutano na watumishi wa Manispaa Songea   leo tarehe 23 disemba 2020 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Mh.Jafo alianza kuipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa kazi nzuri ya ujenzi wa barabara km 10.3  ambazo zimejengwa kwa kiwango kizuri cha Rami kwa kuzingatia  uwepo wa miundombinu  ya  mifereji na taa. Amewataka wananchi kuendelea  kuzitunza barabara hizo na kutoruhusu kutupia takataka.

Manispaa ya Songea na Halmashauri nyingine zinaingizwa katika miradi mingine ya miji 45 na kufanya uboreshaji mkubwa wa miundombinu ya Barabara. Mpango wa Serikali katika Miji 45 utakuja kufanya kazi nyingine kubwa katika Manispaa ya Songea. Kwa hilo ondoeni shaka. Alisema Mh. Jafo.

Aliongeza kuwa  uwekezaji huu utasaidia Halmashauri kupata mapato makubwa Zaidi pamoja na kutanua uwigo wa biashara kwa  utoaji wa nyama bora kwenda Nchi nyingine za jirani.

Akimpongeza Kaimu Mhandisi Manispaa ya Songea  Caroline M. Bernard kwa usimamizi mzuri wa   ujenzi wa barabara, machinjio mpya ya kisasa, na stendi ya mabasi Tanga, ambapo alibainisha kuwa   kutokana na kuridhishwa na utendaji wake alishauri angepandishwa daraja na kuwa mkuu wa Idara.

Amewataka viongozi na wataalamu kufanya kazi kwa ushirikiano wa   kukusanya mapato  ya Serikali kwa kuacha migogoro isiyo na tija  ndani ya Halmashauri  ili kukusanya mapato hayo kufikia 50% kila Halmashauri ifikapo januari 15 2021.  Alisema hakuna mtu aliyetulazimisha katika upangaji wa bajeti, na ikiwa bajet tumeipanga wenyewe, mipango ya kwetu wenyewe, hakuna sababu ya kufeli kukusanya mapato. “alisisitiza mh. Jafo.”

Aidha, katika utoaji wa mikopo  ya 10% inayosimamiwa na  maendeleo ya jamii kwa kupitia vikundi vya   vijana 4%, wanawake 4%  na walemavu 2%  inatakiwa kutoa kipaumbele kwa vikundi vya  wajasiliamali  ili waweze kunufaika na mikopo inayotolewa yenye riba nafuu na Serikali kwa lengo la kukuza mitaji yao.

Alisema “ nanukuu “ Kumbukeni hotuba ya Mh. Rais ya novemba 20 mwaka 2015, wakati anazindua Bunge la 15, ukiachilia agenda ya ufisadi na wizi, jambo jingine ni uzembe uliopitiliza kwa watumishi wa mamlaka ya Serikali za Mitaa , alikuwa hapendezwi kabisa na utendaji wa kazi, uzembe wa ukusanyaji mapato, na miradi isiyokizi kiwango.” Mwisho wa kunukuu”

Naye Kaimu  Mhandisi wa Manispaa ya Songea Caroline M. Bernard alisema Mradi wa ujenzi wa machinjio kwa awamu ya kwanza umegharimu 2,748,850,900.00 ambapo kwa awamu  ya pili mradi wa machinjio ulianza kutekelezwa tarehe 11 januari 2020 na unatarajiwa kukamilka 30 disemba 2020 na hadi kukamilika utagharimu 5,748,799,559.00.

Caroline alibainisha kuwa mradi wa ujenzi wa kituo kikuu cha mabasi Tanga ulianza kutekelezwa tarehe 25.03.2018 na umekamilika tarehe 12.02.2020 kwa gharama ya shilingi 6,887,083,722.60.  Mh. Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Katika kikao cha  ufunguzi wa baraza la madiwani kilichofanyika 16 disemba 2020 aliliagiza baraza la madiwani kuhakikisha kituo hicho cha mabasi kinafanya kazi kwa ufanisi kuanzia 01 januari 2021.

Naye Mstahiki Meya Manispaa ya Songea Michael Leodgar Mbano alisema kupitia agizo lililotolewa na Mkuu wa Mkoa katika Mkutano wa baraza la Madiwani wameanza kutekeleza leo 23 disemba kwa kuitisha kikao cha wadau  ili waweze kutekeleza agizo hilo.

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

23 disemba 2020.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa