• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MH.ISSA MKWAWA DIWANI KATA YA MATOGORO MANISPAA YA SONGEA, ATOA ZAIDI YA TSH. 1,200,000 MOTISHA KWA WALIMU NA WANAFUNZI.

Tarehe ya kuwekwa: March 8th, 2021

Diwani wa kata ya Matogoro  Issa S.Mkwawa amefanya tafrija fupi ya kuwapongeza walimu wote wa  shule zilizopo katika kata Ya Matogoro  kwa kufaulisha  mtihani wa darasa la saba pamoja na mtihani wa  kidato cha nne 2020.

Mkwawa ametoa pongezi hizo kwa shule za Msingi tatu na Sekondari 2,( Shule ya Msingi Matogoro, Shule ya Msingi Chemchem, Shule ya Msingi Mahilo, Kalembo Sekondari, na Matogoro Sekondari)  kwa lengo la kuwatia moyo  Walimu ambao wamefaulisha vizuri masomo yao  ili waweze kuongeza bidii katika kutekeleza wajibu wao. Tafrija hiyo  ilifanyika tarehe 05/03/2021 katika ukumbi wa chuo cha walimu songea.

Miongoni mwa zawadi zilizotolewa nipamoja na   sukari kilo 10 kwa kila shule, fedha shilingi 40,000/= kwa kila mwalimu aliyefaulisha  vizuri katika masomo, zawadi kwa wanafunzi waliofaulu  daraja la kwanza,na  la pili pamoja na fedha  shilingi 1,200,000 zimetolewa  kwa ajili kulipa  walimu  wawili wa  wahesabu watakao jitolea kufundisha hesabu  kwa muda wa miezi sita kwa sekondari ya Kalembo na Matogoro.

Alisema baada ya kubaini kuwepo kwa changamoto za ukosefu wa walimu wa hisabati wakati Serikali ikifanya utaratibu wa kutatua changamoto hiyo, Kiongozi huyo makini aliamua kulipa kiasi hicho cha fedha shilingi laki sita kila sekondari kwa ajili ya malipo ya mwalimu atakayejitolea kufundisha wanafunzi shule ya kalembo na matogoro.

Aliongeza kuwa kilichomvutia ni kuona shule za kata  zinafanya vizuri kwa baadhi ya wanafunzi kfaulu dalaja la juu hatimaye  kushika nafasi ya 18 na 19 Kiwilaya kati ya  shule 36  zilizofanya mtihani wa kidato cha nne  mwaka 2020.  

Alibainisha kuwa Kata ya Matogoro imejipanga vizuri katika kutekeleza ILANI ya Chama Cha Mapinduzi kwa kuanza  kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi ikiwemo na  miundombinu ya shule, vivuko, zahanati na majengo ya kiutawala  kwa kuwashirikisha wananchi/wadau mbalimbali ili kufikia malengo yaliyokusudiwa pamoja na kuweka mpango shirikishi jamii kwa wananchi wenyewe wa kuibua  miradi kipaumbele.

Mkwawa alisema hadi hivi sasa kata hiyo imeshajenga nyumba ya Mganga moja  ambayo ipo hatua ya ukamilishaji ambayo imejengwa kwa nguvu za wananchi  katika Zahanati ya Mahilo, pamoja na ujenzi wa ofisi ya Mtaa Mkwawa ambayo ipo hatua ya Renta ambayo imejengwa kwa nguvu za wananchi.

Alitoa rai kwa wananchi, wazazi  na kamati za shule kuendelea kutoa ushirikiano  kwa walimu ili kuleta maendeleo mazuri ya wananfunzi. Ameahidi kuendelea kutoa zawadi kwa shule zake zote ndani ya kata hiyo kila mwaka ili kuwatia moyo walimu   kwa kufanya kazi vizuri.

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

08 MACHI 2021.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa