• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MIAKA 62 YA UHURU TANZANIA BARA YENYE MAFANIKIO

Tarehe ya kuwekwa: December 9th, 2023

9 Disemba ni siku ya Maadhimisho ya Uhuru Tanzania Bara ambayo huadhimishwa  kila mwaka kwa lengo la kukumbuka historia ya harakati za uhuru wetu na kwa mchango wa viongozi wetu.

Awali Tanganyika ilijumuisha Rwanda na Burundi kuunda koloni la Mjerumani hadi mwaka 1914 ambapo ulikuwa mwisho wa vita vya kwanza vya dunia. Kuanzia tarehe 20 Julai, 1922 Tanganyika ilirasimishwa na kuwa chini ya mamlaka ya shirikisho la Mataifa (League of Nations) chini ya Uingereza.

Kwa upande wa Zanzibar, Historia inahusu eneo ambalo linaundwa na Jamhuri ya watu wa Zanzibar ambayo ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo  Eneo hili la Zanzibar lilipata uhuru kwa kufanya mapinduzi dhidi ya utawala wa Sultani na kuweka uongozi wa waafrika chini ya Chama cha ASP mwaka 1964 kilichoongozwa na Sheikh Abeid Amani Karume na ilipofika    tarehe 26 Aprili, 1964 Tanganyika na Zanzibar ziliungana na kuunda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Aidha, Baada ya Uhuru Tanganyika ilishuhudia mabadiliko mengi ya kisiasa ikiwa ni katika juhudi za kujipatia maendeleo na kuondoa mabaki ya utawala wa mkoloni  ambapo viongozi wa Tanganyika waliunda Katiba iliyojikita kwenye mahitaji ya nchi mpya ambayo yalilenga mgawanyo wa mamlaka ya kisiasa na majukumu mbalimbali ya viongozi pamoja na wananchi.

Katika kuadhimisha Sherehe hii Manispaa ya Songea imeweza kufanya  shughuli mbalimbali kuanzia tarehe 01 Disemba hadi 09 Disemba  kwa kufanya usafi wamazingira katika eneo la soko la Mjimwema, kushiriki  Michezo pamoja na  kupanda miti katika eneo la Shule ya Chief Zulu Academy ambapo zoezi hilo liliongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanal. Laban Thomas katika kilele cha maadhimisho hayo.

Kanal. Laban akizungumza na wananchi kwenye kongamano la kilele cha maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru Tanzania bara alisema” Mafanikio tunayoyaona  yametokana na juhudi na nia ya dhati ya viongozi wetu walioongoza Taifa hili na wanaoendelea kuliongoza.”

Amesema “tunaposherehekea siku hii muhimu kwa namna ya pekee tumkumbuke kiongozi wa kwanza wa Taifa letu Marehemu Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage  Nyerere kwa kazi kubwa aliyoifanya na kuwaongoza watanzania  wakati wa kudai uhuru na kuhakikisha tunakuwa huru na kuunda Taifa hili wakati huo iliitwa Tanganyika.”

Amewataka wazazi na walezi wote kuhakikisha wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza kwa mwaka wa masomo 2024 wahakikishe wanaripoti shule mara baada ya kufungua shule.        “ Alisisitiza”

Kwa upande wa Manispaa ya Songea katika Sekta ya Elimu wakati  wa Uhuru mwaka 1961 kulikuwa na  Shule za Msingi sita zilizojengwa na Mkoloni ambazo ni Shule ya Msingi  Matogoro – 1949, Shule ya Msingi Ruhila – 1929, Shule ya Msingi Tanga,  Shule ya Msingi Lilambo, Shule ya Msingi Sinai na  Shule ya Msingi Mlete.

Aidha, Baada ya Uhuru Maendeleo ya sekta ya elimu katika Manispaa ya songea tangu Tanzania ilipopata uhuru yamegawanyika katika Idara ya Msingi, Sekondari, vyuo vya kati na elimu ya juu, ambapo kwa upande wa Elimu Msingi Hata hivyo hadi kufikia   mwaka 2023, halmashauri ya   Manispaa ya Songea ina jumla ya shule za Msingi 101, ambapo shule 84 ni za Serikali na 17 ni za Taasisi binafsi (Private), sawa na ongezeko la 1583%.

Kwa upande wa Sekondari Wakati wa uhuru kulikuwa na shule ya sekondari 01 ambayo ilikuwa inamilikiwa na Serikali ambayo ni  shule ya Wavulana ya Songea Boys iliyoanzishwa mwaka 1950 na serikali ya wakoloni kwa lengo la kuandaa viongozi watakao tawala pindi nchi itakapopata uhuru  ambapo Mwaka 1961 shule hiyo  ilikabidhiwa kwa Serikali ya Tanganyika.

 Kuanzia miaka ya 2000 kutokana na Mpango wa Serikali wa kupanua Elimu kwa kujenga shule za  kata ambapo shule zimeongezeka hadi kufikia,  2023 Manispaa ya Songea ina idadi ya shule za sekondari 43 zikiwemo za serikali  26 na zisizo za serikali 17.

Kwa upande wa sekta ya  afya  baada ya Uhuru Katika manispaa ya Songea, imeweza kufanikiwa ya kujenga Vituo vya kutolea huduma za afya, wigo wa upatikanaji wa huduma za afya, Watumishi wa kada za wataalamu wa afya na Huduma ya chanjo.

Miongoni mwa mafanikio katika Sekta ya Afya baada ya Uhuru ni pamoja na kuongezeka kwa  Vituo 60  vya kutolea huduma za afya  ngazi zote  ikilinganishwa na kituo kimoja (1) mwaka 1960,

Kwa Upande wa huduma za miundombinu ya barabara Wilaya ya Songea baada ya Uhuru hadi sasa imefanikiwa kuwa na mtandao wa barabara wenye jumla ya kilometa 2200.586 kati ya hizo, Kilomita 60.252 ni barabara  za  lami pamoja na taa za barabarani, kilomita 525.897 ni barabara za Changarawe, kilomita 1614.437 ni barabara za udongo na madaraja 150.

Hata hivyo baada ya  uhuru hali ya barabara imeimarika kwa kiasi kikubwa ambapo kwa sasa mtandao wa barabara katika wilaya ya Songea imegawanyika katika makundi matatu ikiwemo na  kilometa 1023.29 sawa na asilimia 46.5 za barabara zina hali nzuri, kilometa 307.91 sawa na asilimia 14 zina hali ya kuridhisha na kilomita 869.386 zina hali isiyoridhisha sawa na asilimia 39.5.

Kwa upande wa maji katika Manispaa ya Songea Mtandao wa bomba za usambazaji majisafi umeongezeka kutoka km 24 hadi km 568.511, Idadi ya wateja wa majisafi imefikia 22,343 ambao wote wamefungiwa dira za kupima maji, Mamlaka inayo matenki 11 yenye ujazo wa meta za ujazo 4,785 kati ya mahitaji ya meta za ujazo 20,593, pamoja na Uboreshaji wa mfumo wa ulipaji ankara za maji.

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI












Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa