• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MIAKA MIWILI YA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN " SONGEA MC "

Tarehe ya kuwekwa: March 17th, 2023

Halmashauri ya Manispaa ya Songea inatoa shukrani  kwa Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha Bil. 9  kwa ajili ya utekelezaji wa miundombinu ya Elimu Msingi na Sekondari katika kipindi cha miaka miwili 2021 hadi 2023 katika  Manispaa ya Songea.

Halmashauri ya Manispaa ya Songea  imepata mafanikio makubwa kupitia Sekta ya Elimu ambapo imesaidia kupunguza changamoto ya madarasa 142 pamoja na madawati au viti na meza  sambamba na utoaji wa elimu BURE kuanzia shule ya awali hadi kidato cha sita. TUNASHUKURU.

Hayo yamejilii katika kikao cha waandishi wa Habari kilichofanyika leo tarehe 17 machi 2023 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea kwa lengo la kutoa taarifa kwa waandishi wa habari juu ya mafanikio ya utekelezaji wa miaka miwili ya Rais wa awamu ya sita Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Kikao hicho kimeongozwa na  Mstahiki Meya Manispaa ya Songea Michael Mbano ambaye amesema” katika kipindi cha awali Manispaa ya Songea ilikuwa na vituo vya afya viwili ambapo mara baada ya uongozi wa awamu ya sita Manispaa ya Songea  imejenga  vituo vya afya vinne ikiwemo na kituo cha afya Lilambo kilichojengwa kwa mapato ya ndani, kituo cha afya Mletele, kituo cha afya Subira na kituo cha afya Msamala  kwa gharama ya Bil. 3.550. ‘Alipongeza”

Mhe. Mbano aliongeza kuwa katika Sekta ya kilimo kwa mwaka 2022/2023 Manispaa ya Songea imefanikiwa kupokea  Pembejeo ya RUZUKU  Tan 15,487 kwa wakulima 137,487 ambapo ongezeko hilo limetokana na Serikali kuweka Ruzuku ya Mbolea kwa Mkulima.

Akizungumzia kuhusu Sekta ya Barabara katika Manispaa ya Songea ilipokea kiasi cha Bil. 6.133 kwa ajili ya ukamilishaji wa miundombinu ya barabara, madaraja na mifereji  hususani katika barabara ya Lami Kata ya Seedfarm, Lizaboni, kata ya Bombambili Sanga one hadi Ujenzi. “Alibainisha.”


 Aidha, Bil. 1.2 zimetolewa na Halmashauri kwa ajili ya kuvikopesha vikundi mbalimbali vya wajasiliamali wadogo kwa wanufaika wa vikundi vya wanawake 4%, Vijana 4% na  walemavu  2% fedha hizo ni mafanikio ya makusanyo ya mapato ya ndani ya  10% pamoja na Kaya 5611 zimenufaika na Mfuko  wa TASAF kwa watu wasioweza kujikimu ili kuondoa umaskini katika kaya kwa ujumla..


Katika kutekeleza shughuli za Mpango na Mikakati ya kimaendeleo  Serikali imefanikiwa kusimamia zoezi la SENSA ya Watu na Makazi  na POSTI KODI ambapo kwa Manispaa ya Songea ina jumla ya wakazi  286,285  hii itasaidia kupanga mipango ya maendeleo ikiwemo na kufahamu mahitaji halisi ya kijamii.

Alipongeza Serikali ya awamu ya Sita kwa kutoa fedha  Zaidi ya Bil. 145 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa maji ambayo ni sehemu ya  utekelezaji wa mradi wa miji 28 kwa ajili ya kumtua mama ndoo kichwani ambapo kwa Manispaa ya Songea itawezesha kuondoa kero ya maji kwa asilimia 95%. “Mhe. Mbano Aliongeza”.

Aliongeza kuwa Manispaa ya Songea inatarajia kuanza utekelezaji wa miradi ya Masoko mawili ya  kisasa Manzese A na Manzese B, pamoja na ujenzi wa kiwango cha Lami KM 10.5  ambao Unatarajia kujengwa hivi karibuni pamoja na ujenzi wa  chuo kikuu cha Uhasibu Arusha katika Kata ya Tanga.

 

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.






Matangazo

  • MATANGAZO mbalimbali ya Manispaa ya Songea kwa njia ya Redio January 31, 2020
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Januari 2020 January 25, 2020
  • MATANGAZO muhimu kwa wakazi wa Manispaa ya Songea January 31, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MIAKA MIWILI YA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN " SONGEA MC "

    March 17, 2023
  • BIL 145.77 KUTATUA CHANGAMOTO ZA MAJI MJI WA SONGEA.

    March 11, 2023
  • YALIYOJIRI SIKU YA WANAWAKE DUNIANI MKOANI RUVUMA

    March 09, 2023
  • DC Songea ameitaka Jamii kupinga Ukatili wa Kijinsia

    March 02, 2023
  • Tazama zote

Video

BIL. 145.77 KUTATUA CHANGAMOTO ZA MAJI MJI WA SONGEA
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa