• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MIL. 108.6 ZATOLEWA MIKOPO KWA WANAWAKE, VIJANA, NA WALEMAVU - MANISPAA YA SONGEA

Tarehe ya kuwekwa: December 31st, 2020

Milion 418,436,332/=  za daiwa  kutorejeshwa mkopo wa vikundi vya wanawake 4%, vijana 4%, na walemavu 2% sawa na asilimia 10%,  fedha ambazo kama zingerejeshwa kutoka kwenye vikundi hivyo zingeweza kukopeshwa kwa wanavikundi wengine.

Kauli hiyo imetamkwa na   katibu Tawala wa Wilaya ya Songea Pendo Daniel  katika mafunzo yaliyofanyika tarehe 30 disemba 2020 katika ukumbi wa manispaa ya Songea kwa lengo la kuidhinisha utoaji wa mikopo kwa wanavikundi 52 ikiwa wanawake vikundi 26, vijana vikundi  20 na walemavu vikundi 6.

Pendo, alitoa pongezi kwa Halmashauri ya Manispaa ya Songea  kwa kutoa mikopo kwa wanavikundi kiasi cha shilingi 108,669,444.08 kwa mwezi disemba  kwani sio kila Halmashauri inauwezo wa kutoa mikopo hiyo kwa wanavikundi.

 Amewataka wanavikundi wote wanaodaiwa  mkopo huo kufanya marejesho ya fedha  418,436,332/=  walizokopa ambazo bado hazijarejeshwa, endapo hawatarejesha fedha hizo, watachukuliwa hatua za kisheria.

Naye Mstahiki Meya Manispaa ya Songea Michael Mbano alisema  tumeanza kutekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi  kwa kuanza kutoa mikopo kwa wanavikundi ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya CCM katika kipindi cha 2025.

 Mbano ametoa rai kwa wanavikundi hao kutekeleza makubaliano yao  kadili ya maandiko waliyokubaliana ikiwemo na kufanya marejesho ya mkopo kwa wakati ili waweze kukopeshwa wanavikundi wengine.

Alieza bayana kuwa “ Serikali hii haipendi udanganyifu, uongo, na utapeli na  endapo utachukua fedha za Serikali ambayo imekusaidia kutoka hatua moja kwenda hatua nyingine lakini hutekelezi kwa maksudi jukumu lako la kulipa deni basi hauna tofauti ya mwizi yeyote yule.”  Alisisitiza Mbano.

Naye kaimu Afisa Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Songea Mensa Ngelangela  katika hotuba yake iliyosomwa kwa mgeni Rasmi alibainisha kuwa mwezi disemba 2020 mikopo iliyotolewa kwa wanavikundi wanawake 4%  kiasi cha 16,000,000/=,  vikundi vya vijana kiasi cha 16,000,000/=  na vikundi vya  walemavu kiasi cha 8,000,000/=.

Mensa aliongeza kuwa fedha za marejesho zikiwa na mgawanyo wa asilimia  4% wanawake shilingi 12,000,000 na asilimia 4% vijana 12,000,000 na 20%  watu wenye ulemavu 6,000,000 pamoja na bakaa zikiwa na mgawanyo wa 4% wanawake  shilingi 15,467,777.912, asilimia 4% vijana shilingi 15,467,777.912 na walemavu shilingi 7,733,883.96.

Katika kutatua changamoto za wadaiwa wa mkopo, Idara ya maendeleo ya jamii imeweka mikakati ya kufanya uhakiki wa vikundi vyote vinavyoomba mkopo,  kabla ya kupewa mkopo huo watatakiwa kwenda kukagua miradi yao  ili kujiridhisha na vikundi hivyo.

Naye Mkuu wa TAKUKURU Wilaya ya Songea Amos Lugomela alisema kazi yao ni kuchunguza na kushauri namna ya kuzuia mianya ya rushwa, na wale wote wanaochunguzwa, ushahidi ukipatikana wanafikishwa mahakamani ili waweze kujibu mashitaka yanayowakabili.

Lugomela alisema kwa mujibu wa semina hiyo ya utoaji wa mikopo kwa wajasiliamali alibainisha kuwa Serikali za mitaa zote kisheria zinapaswa kutenga  10% kawajili ya vikundi vya wanawake 4%, vijana 4%, na walemavu 2%, hiyo ni kwasababu ya kuleta maendeleo kwa wanannchi wake.

Ametoa rai kwa wale wote waliokopa mikopo hiyo  na hawajarejesha mikopo yao ambayo ni jumla ya shilingi milioni 418,436,332 ambazo zindaiwa kutorejeshwa na wanavikundi, walipe mara moja na endapo hawatarejesha fedha hizo watachukuliwa hatua za kisheria.

Amewataka Maafisa Maendeleo ya jamii baada ya kutolewa mikopo hiyo kwa wanavikundi watatakiwa kupeleka majina ya wanavikundi waliokopa sasa na wadaiwa wote  yakionyesha mahali wanapoishi na shughuli wanazozifanya ili waweze kufuatiliwa.

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

31 disemba 2020.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Chupa 14,789 za Damu Kukusanywa Mkoani Ruvuma

    June 04, 2025
  • Mazishi ya Muasisi wa TANU Alhaji Mustapha Songambele

    June 03, 2025
  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • Tazama zote

Video

katibu Mkuu CCM Taifa Aongoza Maziko ya Alhaji Songambele
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa