• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Milion 113 Zatolewa Mkopo kwa Vikundi 48 Manispaa ya Songea.

Tarehe ya kuwekwa: June 29th, 2021

Manispaa ya Songea imetoa kiasi cha Tshs 113, 760, 000/= kwa jumla ya  Vikundi vya wajasiliamali  48 vyenye wanachama 144 ikiwa vikundi vya wanawake 39, vikundi vya vijana 07 na vikundi vya watu wenye ulemavu 2.

Mikopo hiyo imetolewa ikiwa ni makusanyo ya fedha zitokanazo na mapato ya ndani ambapo wanawake asilimia 40%, vijana 40% na walemavu asilimia 20%, tukio hilo limefanyika leo tarehe 29 Juni 2021 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea, kwa lengo la kuwainua wajasiliamali wadogo waliopo katika Manispaa ya Songea.

Mgeni rasmi katika zoezi hilo la utoaji wa mikopo kwa vikundi 48 alikuwa  Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini Dkt. Damas Ndumbaro Waziri wa Utalii na Maliasili  ambaye aliwakilishwa na Naibu Meya Jeremia Mlembe ambapo aliipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa kuonyesha juhudi katika kutekelezaji wa sheria na kanuni za uchangiaji wa 10% ya mapato ya ndani pamoja na uhimizaji wa utoaji wa mikopo ambapo kiasi cha Tshs. 113,760,000/= zimetolewa.

Jeremiah alisema  Mkopo huu utumike kwa ajili ya miradi yenu kulingana na  maandiko ya miradi iliyoombwa ili  iweze kuleta  Mafanikio ya haraka kwa jamii sambamba  na kufanya marejesho mkopo  kila mwezi na kwa wakati ili kuwapatia fursa wahitaji wengine kukopeshwa na endapo hawatarejesha kwa wakati watachukuliwa hatua za kisheria. ’Alisisitiza’

Amewata  wajasiliamali  hao  kujitokeza kwenda kupima afya kwa hiari, kujilinda  na janga la UKIMWI pamoja na CORONA.’ Jeremia  alieleza’

Kwa upande wake Afisa maendeleo ya jamii Manispaa ya Songea Martin Mtani amesema  kabla ya kutoa mkopo huo timu ya wataalamu ilifanya ufuatiliaji na uhakiki kwa vikundi vyote vilivyoomba mikopo na baadhi ya miradi ya vikundi vilivyokidhi vigezo ni ufugaji wa kuku, nguruwe, ushonaji, ufumaji wa makapu na utengenezaji batiki.

Mtani aliongeza kuwa utoaji wa mikopo hiyo umewasaidia  wanufaika  wengi kuweza kuboresha makazi yao, kusomesha watoto na kutoa ajira kwa watu wengine.

Amesema kuwa kwa mwaka wa fedha 2021/2022 Halmashauri ya Manispaa ya Songea inatarajia kuboresha utaratibu wa utoaji wa mikopo mikubwa kwa vikundi vyenye miradi yenye tija ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Mheshimiwa Rais  wa Jamhuri  ya Muungano wa Tanzania.’Alibainisha’

IMEANDALIWA NA,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA,

29.06.2021.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa