• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MILIONI 164, ZATOLEWA KWA AJILI YA UKARABATI WA MAKUMBUSHO YA DR. KAWAWA.

Tarehe ya kuwekwa: August 14th, 2020

Hayo yamebainika katika ziara ya Waziri wa Habari Sanaa,  Michezo na Utamaduni Dr Harrison Mwakyembe iliyofanyika 12-13/08/2020 Manispaa ya Songea.

Mwakyembe alisema lengo la ziara ni kutembelea kituo cha Redio TBC Taifa kwa ajili ya kufanya ufuatiliaji wa  usikivu wa Redio ya Serikali na kubaini kama kuna changamoto ambazo zinakwamisha utandaji bora wa Mitambo hiyo ambapo aliweza kutembelea Mitambo ya TBC Taifa iliyopo katika milima ya Matogoro, kituo cha Redio Jogoo,na  Key  FM pamoja na maeneo ya urithi wa ukombozi yaani makumbusho ya Majimaji MKoani Ruvuma.

Awali TBC Taifa ilikuwa na changamoto ya usikivu  kwa baadhi ya maeneo Mkoani Ruvuma lakini kupitia mitambo iliyowekwa Matogoro imesaidia kuondoa tatizo hilo  ambapo kwasasa TBC Taifa inasikika vizuri bila tatizo lolote.

Hakusita kuwapongeza wamiliki wa Redio zilizopo ndani ya Manispaa ya Songea  Key FM, na Jogoo FM kwa uwekezaji mzuri  ambao pia wamesaidia kutoa ajira kwa jamii pamoja na kuliongezea pato  Taifa letu (Kodi).

Alibainisha kuwa taalma ya uandishi wa habari ni taalma muhimu ambayo huzingatia sheria, kanuni na maadili  katka kuichakata  habari  kitaalamu na kuitoa kwa jamii  bila kukiuka miiko ya taalma hiyo. Pia aliongeza kuwa mwandishi wa habari ni  Mwalimu, Mchambuzi wa habari, hufanya kazi ya  kutafuta habari na kuripoti kitu chochote kilichotokea  katika  jamii.

Akizungumzia kuhusu  michezo, alisema  ni  muhimu sana  kuibua vipaji vya watoto wazawa  ili kuwaandaa kimichezo hapo baadae na hatimaye tutaweza kuachana na dhana ya kuwategemea wachezaji wa kigeni ambao vipaji vyao ni vya kawaida. Alisistiza.

Aliongeza kuwa msimu ujao wa michezo atahitaji kuona kwamba mchezaji wa  nje yeyote atakayesajiliwa  kucheza  Tanzania atatakiwa kuwa na sifa thabiti na  awe anacheza ligi kuu kwao au  timu ya Taifa lake, au awe anahistoria ya kucheza kwenye timu zilizopo kati ya 50 bora.

Alisema amepokea changamoto ya uhaba wa maafisa michezo Mkoani Ruvuma  ambapo alisema ni Halmashauri Tunduru pekee yenye Afisa michezo kati ya  Halmashauri nane zilizopo Mkoani Ruvuma, na ameahidi kulifanyia kazi.

Naye Mhifadhi wa Makumbusho ya Majimaji Mkoa wa Ruvuma Adson Ndyanabo alisema” nanukuu” Makumbusho ya Taifa la Tanzania inapenda kuishukuru Serikali ya awamu ya tano (5) chini ya Mh. Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwakutupatia Zaidi ya Tshs 164,000,000/= kwa ajili ya ukarabati wa Makumbusho ya Dkt. Kawawa kazi inayosimamiwa na wakala wa majaengo (TBA) kwa ajili ya kuboresha miundombinu.”mwisho wa kunukuu.

IMETAYARISHWA NA;

AMINA PILLY

KAIMU AFISA HABARI –MANISPAA YA SONGEA.

 14.08.2020.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa