• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MILIONI 220 kukarabati mabweni mawili Songea Girls

Tarehe ya kuwekwa: May 24th, 2018

SHULE ya sekondari ya wasichana Songea(Songea Girls) imepewa na serikali shilingi milioni 220 za awamu ya kwanza kwa ajili ya kukarabati mabweni mawili.

Mkuu wa shule hiyo Tupoke Ngwala amewaambia wanahabari ambao wamefanya ziara ya kutembelea shule hiyo kuwa ukarabati huo unafanywa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) ambapo tayari wamekabidhi bweni moja la ghorofa ambalo  limekarabatiwa kwa zaidi ya shilingi milioni 102.

Ngwala amesema bweni hilo ambalo linaitwa Mputa ni la ghorofa likiwa uwezo wa kuchukua wanafunzi 110 na kwamba hivi sasa kazi inayoendelea ni ya ukarabati wa bweni la pili linaloitwa Zulu.

“Ukarabati wa bweni lililomalizika ulianza Januari 10 mwaka huu  na kwamba ukarabati wa bweni la pili umeanza tangu Aprili mwaka huu,lengo ni kukarabati mabweni yote matano kwa awamu’’,anasisitiza Ngwala.

Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa shule serikali imetoa zaidi ya shilingi bilioni 1.6 kwa ajili ya kufanyia ukarabati majengo yote ya shule hiyo yakiwemo mabweni na majengo ya utawala ili kuhakikisha shule hiyo inakuwa na mazingira mazuri ya kujifunzia na kufundishia.

Hata hivyo amesema kabla ya serikali kutoa fedha hizo mabweni yalikuwa na hali mbaya ambapo kulikuwa na msongamano mkubwa wa wanafunzi ambao walikuwa wanalala katika vitanda vilivyochakaa ambapo serikali pia imetengeneza vitanda vipya 110 katika bweni ambalo limekamilika.

Shule ya sekondari ya wasichana Songea ni miongoni mwa shule kongwe nchini ina wanafunzi 874 wanaosoma kidato cha tano na sita ambayo ilianzishwa mwaka 1974.

Imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Mei 24,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa