• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MIRADI 6 YENYE THAMANI YA BIL. 25 YATEMBELEWA NA MWENGE - SONGEA MC

Tarehe ya kuwekwa: June 15th, 2024

MWENGE wa Uhuru 2024 ukiwa Halmashauri ya Manispaa ya Songea  umepita katika tarafa 2, kata 13, Mitaa 39  na umekimbizwa umbali wa  KM  98.2  ambapo umepita katika  miradi 9 ikiwemo na kuweka jiwe la msingi katika  miradi miwili, ugawaji wa  vifaa katika mradi mmoja, na kutembelea miradi 6 yenye jumla ya  Shilingi Bil. 25, 193,941,237.30.

Hayo yamejiri wakati wa kukabidhi Mwenge wa Uhuru katika kijiji cha Mtyangimbole Halmashauri ya Madaba ambapo Mwenge wa Uhuru uliwasili Manispaa ya Songea  tarehe 14 Juni 2024 na kupokelewa  na Mkuu wa Wilaya ya Songea Mhe. Kapenjama Ndile  ukitokea Wilaya ya Mbinga.

Kiongozi waMbio za  Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2024 Godfrey Mnzava amewataka wananchi  kushiriki kikamilifu katika utunzani mazingira na kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, kutunza amani katika maeneo yote hususani katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi,  mapambano dhidi ya dawa za kulevya, Malaria, ukimwi, Rushwa pia amesisitiza Lishe bora na siyo kujaza tumbo.

Akitoa taarifa  ya miradi mbalimbali kwa kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2024, Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Wakili. Bashir Muhoja amesema” Manispaa ya Songea ni miongoni mwa Halmashauri 12 zilizobahatika kupata miradi wa ubaoreshaji wa miundombinu ya barabara za lami nzito zenye urefu wa KM 10.1 yenye jumla ya barabara 20 za lami katikati ya Mji wa Songea wenye thamani ya zaidi ya Bil. 22  ambao umefadhiliwa na Jumuiya ya Maendeleo ya kimataifa (IDA) kupitia Benki ya Dunia kwa ajili ya uboreshaji wa miundombinu na ushindani wa Miji, Manispaa, Majiji Nchini Tanzania  (TACTIC) ambao  unaratibiwa na Ofisi ya Rais TAMISEMI ambao umefikia asilimia 20 ya utekelezaji wa barabara  hiyo.

Aidha miradi mingine iliyotembelewa na mwenge wa uhuru ni mradi wa maji katika kata ya Tanga Mtaa wa Pambazuko Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma ambao umegharimu shilingi 778,149,730 unaotarajia kuhudumia watu 15,990.


Miradi miwili  iliyowekwa jiwe la Msingi ni  ujenzi wa nyumba ya Mkurugenzi unaogharimu  Shilingi  Mil. 180 hadi utakapokamilika, pamoja na ujenzi wa vyumba vya madarasa  10 na matundu 10 ya vyoo  yenyejuml ya  thamani ya Mil. 259,500,000 katika shule ya Sekondari Londoni ambapo  shule hiyo ilianzishwa  mnamo 2004 ina wanafunzi wanaosoma kidato cha kwanza hadi kidato cha sita wapatao 1,399 pia kukamilika kwa mradi wa vyumba 10 vya madarasa  utawezesha kurahisisha  mbinu za ufundishaji na ujifunzaji kwa wanafunzi.

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.  

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa