• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MIRADI YA UVIKO 19 KUTEKELEZWA KWA ASILIMIA 95% MANISPAA YA SONGEA.

Tarehe ya kuwekwa: December 7th, 2021

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

07.12.2021

Halmashauri ya Manispaa ya Songea yafikia asilimia 95% ya utekelezaji wa miradi ya mpango wa maendeleo kwa ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya UVIKO-19.

Hayo yamebainishwa na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea Michael Mbano leo tarehe 07 Novemba 2021 wakati akizungumza na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali ndani ya Mkoa wa Ruvuma pamoja na wataalamu mbalimbali kutoka Manispaa ya Songea kwa lengo la kujulisha umma juu ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ambayo inaendelea kutekelezwa pamoja na kutolea ufafanuzi juu ya mipango mkakati iliyopo katika kuboresha Manispaa ya Songea.

Mbano alianza kwa kutoa pongezi kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kutoa kiasi cha shilingi milioni 660,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 26 kwenye shule za sekondari na Msingi  zilizopo ndani ya Manispaa ya Songea ikiwa ni utekelezaji wa Mpango wa maendeleo ya ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya UVIKO-19.

Aliongeza kwa kuwapongeza viongozi pamoja na wataalamu kwa kusimamia na kuhakikisha miradi hiyo inatekelezwa kwa wakati ndani ya mwezi mmoja na katika ubora unaotakiwa, ambapo hadi kufikia tarehe 10 Disemba 2021 Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea ataikabidhi miradi hiyo kwa Mkuu wa Wilaya ya Songea, na ifikapo tarehe 15 Disemba 2021 miradi hiyo itakabidhiwa rasmi kwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma.’Alibainisha’

Alieleza kuwa utekelezaji wa miradi hiyo umesaidia katika kufungua uchumi wa wananchi hasa katika maeneo ambayo ujenzi unafanyika kwa kutoa ajira kwa vijana pamoja na kutoa fursa kwa wafanyabiashara wa vifaa vya ujenzi ndani ya Manispaa ya Songea kuuza bidhaa zao kwa malipo ya uhakika.

Mbano aliendelea kubainisha kuwa pamoja na utekelezaji wa miradi hiyo, Halmashauri ya Manispaa ya Songea inaendelea na ujenzi wa kituo cha afya katika kata ya Lilambo kwa kutumia fedha za mapato ya ndani yanayokusanywa pamoja na ujenzi wa kituo cha afya katika kata ya Msamala  na kata ya Subira ambavyo vinajengwa kwa fedha kutoka Serikali kuu ambapo utekelezaji wa miradi hiyo ipo katika hatua ya msingi.

Aidha, alisema kuwa moja ya mpango mkakati uliopo ni kuboresha huduma za afya, elimu na miundo mbinu ndani ya Manispaa ya Songea ili kuhakikisha inatoka katika hadhi ya kuwa Manispaa na kufikia hadhi ya kuwa Jiji.’Mbano alisisitiza’

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Manispaa ya Songea Dkt. Amosi Mwenda ametoa rai wananchi wa Manispaa ya Songea kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa UVIKO-19 kwa kuendelea kupata chanjo ambayo inatolewa kwenye vituo vyote vya afya 33 vilivyopo ndani ya Manispaa ya Songea ambapo hadi sasa jumla ya watu elfu 19,700 ambayo ni sawa na asilimia 11.2% tayari wameshapata chanjo hiyo.

Akifafanua kuhusiana na mipango mbalimbali ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Songea Afisa maendeleo ya jamii Martin Mtani amewataka wananchi kutumia fursa zilizopo hasa mikopo inayotolewa na Halmashauri ambapo kila mwaka shilingi milioni 350 zinatolewa kwa ajili ya kuwawezesha wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, fedha ambazo hurejeshwa bila riba.

Aliongeza kuwa kwa mwaka huu Halmashauri imejipanga kutoa mikopo yenye tija kwa wananchi ambapo jumla ya kiasi cha shilingi milioni 450 kitatolewa kwa vikundi mbalimbali kwa ajili ya utengenezaji wa viwanda vya ushonaji nguo, kiwanda cha uchakataji wa asali, kiwanda cha utengenezaji wa batiki pamoja na kiwanda cha mafundi welding ambayo itasaidia kuwainua wajasiriamali na kukuza uchumi wa Manispaa ya Songea.’Alibainisha’

Alisema Halmashauri ya Manispaa ya Songea itakuwa na utaratibu wa kuongea na Waandishi wa Habari kila baada ya miezi mitatu ili kuweza kutoa taarifa mbalimbali za Taasisi pamoja na kutangaza mafanikio yote ya Serikali yaliyotekelezwa na kutangaza miradi ya maendeleo.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa