• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MITI inayogeuka mawe kivutio kipya cha utalii Songea

Tarehe ya kuwekwa: May 13th, 2019

IDARA ya Makumbusho ya Taifa kwa kushirikiana na ofisi ya Maliasili na utalii Mkoa wa Ruvuma imeleta vipande viwili vya magogo yanayogeuka mawe kutoka pori la Selous na kuviweka katika Kituo cha Habari za Utalii cha Mkoa wa Ruvuma kilichopo ofisi za maliasili Mahenge mjini Songea.

Mara baada ya kufunguliwa rasmi Kituo cha Habari za Utalii cha Mkoa wa Ruvuma vipande vya magogo yanayogeuka mawe ni miongoni mwa vivutio adimu vya utalii ambavyo vimewekwa katika kituo hicho na kuvutia wengi wanaotembelea katika Kituo hicho.

 Mkurugenzi wa  Makumbusho ya  Taifa ya Majimaji Balthazar Nyamusya anatoa rai kwa watanzania kutembelea katika Kituo hicho na Makumbusho ya Taifa ya Majimaji ili kujifunza  rasilimali muhimu ya Taifa.

Miti inayogeuka mawe inatoka katika Pori la akiba la Selous lilianzishwa  mwaka 1896 na wajerumani likiwa ni pori la kwanza kutengwa kwa ajili ya uhifadhi wa wanyamapori katika Bara la Afrika na la pili duniani kwa ukubwa baada ya  hifadhi ya pori la Marekani ambalo linaitwa Yellowstone.

Mkurugenzi Mstaafu wa Uhifadhi ambaye pia amewahi kuwa Mkuu wa Chuo cha Wanyamapori Kanda ya Likuyuseka katika Pori la Selous Ngwatura Ndunguru anaitaja Moja ya  jamii ya miti ambayo haijafahamika na kutangazwa ipasavyo  kuwa ni  magogo ya miti iliyogeuka mawe ambayo kitaalam inaitwa fossilized tree trucks .

Kanda ya Kusini ya pori la Selous yaani Kalulu kwa mujibu wa Mhifadhi Kabanda Ismail ina umaarufu wa eneo lenye miti iliyogeuka kuwa mawe.Hali hiyo inatokana na hali ya kijiolojia inayotokea kwa mamilioni ya miaka na kuyageuza masalia ya miti kuwa mawe.

 “Utafiti wa kiikolojia umebaini kuwepo kwa makaa ya mawe ambayo asili yake ni miti.Ukitembelea eneo hilo la mawe ya asili ya miti,utabaini  picha halisi  ya miti yaani matawi na maeneo ambayo matawi yake yalidondoka ambapo alama zake bado zipo hadi sasa hali ambayo inathibitisha ukweli wa kisayansi’’,anasisitiza Mhifadhi Ngwatura.

Utafiti wa kisayansi unaonesha kuwa kivutio cha namna hii huwezi kukipata katika sehemu nyingine  yeyote kusini mwa Jangwa la Sahara zaidi ya pori la Selous.

Hata hivyo utafiti wa kimataifa umebaini miti inayogeuka mawe iliyopo pori la Selous Tanzania inapatikana pia kaskazini mwa Afrika  katika nchi za Misri,Libya na Algeria,pia miti hiyo inapatikana  katika nchi ya Ugiriki na Marekani.

Makala imeandaliwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Apongeza kwa Utekelezaji wa Miradi

    May 05, 2025
  • Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Awataka Waajiri kuzingatia Misingi ya Utawala Bora

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Songea Akizindua Stendi ya Bajaji - Songea
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa