• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKAKATI WA KUWAPANGA WAMACHINGA MKOA WA RUVUMA.

Tarehe ya kuwekwa: October 22nd, 2021

NA,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

22.10.2021

Mkoa wa Ruvuma waandaa mkakati wa kuwapanga wajasiriamali wadogo (Machinga) katika maeneo rasmi ya kufanyia biashara.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Balozi Wilbert Ibuge hapo jana tarehe 21 Oktoba 2021 alipokutana na viongozi mbalimbali wa Halmashauri zote 8, wadau na wafanyabiashara kutoka Mkoani Ruvuma katika ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Ibuge alibainisha kuwa mkakati wa kuwapanga wajasiriamali wadogo katika maeneo rasmi  ni kufuatia utekelezaji wa agizo lililotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ambaye aliwataka wakuu wa Mikoa waratibu zoezi la upangaji wa machinga kwenye maeneo rasmi kwa lengo la kuepuka fujo, vurugu, migogoro pamoja na kudhibiti usafi endelevu wa mji husika.

Aliongeza kuwa viongozi wahakikishe maeneo watakayowatenga kwa ajili ya machinga kufanya biashara zao yanakuwa na miundombinu muhimu kama vyoo, maji na umeme pamoja na kuunda dawati maalumu la kuratibu shughuli za wamachinga kwenye Halmashauri husika ambapo amezitaka Taasisi zote kwenye Halmashauri husika kama TRA, TARURA,RUWASA, TANESCO, TANROADS na LATRA kushirikishwa kikamilifu ili kuweka miundombinu wezeshi ya upangaji wa Mji wa wamachinga katika maeneo rasmi ya biashara.

Alisisitiza kuwa zoezi la kuwapanga wamachinga katika maeneo rasmi ya kufanyia biashara liwe limekamilika ndani ya kipindi cha siku 90 kuanzia mwezi Novemba 2021 hadi tarehe 30  Januari 2022  ambapo amewataka viongozi kufanya kazi kwa uweledi na ifikapo Novemba 30 majadiliano ya uboreshaji kwa kuzingatia uwakilishi wa makundi yote yakiwemo  viongozi wa wamachinga katika kuwashirikisha  kwenye maeneo yao ili kuleta umoja.

Naye Mwenyekiti wa wamachinga Mkoa wa Ruvuma Salumu Sandali Masamaki ametoa shukrani kwa viongozi na Serikali kwa kuwapangia wamachinga maeneo rasmi ya kufanyia biashara ambapo alisema endapo mpango huo utakamilika wataweza kufanya biashara zao kwenye maeneo yenye utulivu na wapo tayari kutoa ushirikiano.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Dkt. Frederick Sagamiko alieleza kuwa Manispaa ya Songea  ina jumla ya wafanyabiashara 13,746 ambapo kati ya hao 2,746  wafanyabiashara wenye leseni na wanaolipa kodi Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Wafanyabiashara 11,000 ambao ni  wafanyabiashara wadogo (Machinga) wanaofanya shughuli za biashara za Nafaka, Matunda, Mboga mboga, urembo, Nguo na viatu, Dagaa na vifaa vya umeme.

Alibainisha kuwa yapo maeneo ambayo wafanyabiashara wadogo wanafanya shughuli za biashara lakini hayajatengwa rasmi na Halmashauri kwa ajili ya Biashara ni pamoja na maeneo yote  yanayozunguka soko kuu la Manispaa na wafanyabiashara wa barabara ya Litunu wanaozuia biashara za maduka, maeneo yote  yanayozunguka soko la Manzese A na B, soko la kuku lililopo eneo la Mtini kwenye kiwanja cha Kanisa la Aglican, soko la viatu lilopo KAURU (kwenye geti la kituo cha Mafuta Kisumapai), Wafanyabiashara wadogo walioko ndani ya Stendi ya Mfaranyaki,soko la dagaa lililopo eneo la Versi (nyuma ya stendi ya Mfaranyaki), Wafanyabiashara wadogo  nyuma ya kituo cha mafuta cha kisumapai pamoja na maeneo mengineyo.

Alisema kuwa Manispaa ya Songea imetenga masoko 3 kwa ajili ya kuwahamishia wafanyabiashara wakubwa wanaofanya biashara za jumla wa Mazao makavu, viazi na viazi, samaki na dagaa ambayo ni soko la mazao msamala, Mfaranyaki, Bombambili na Manzese A kwa lengo la kuwavutia wafanyabiashara wadogo katika masoko hayo, pia Halmashauri imepitia upya maeneo ambayo yalitengwa kwa ajili  ya wafanyabiashara na kutenga maeneo mapya pamoja na kuongeza masoko ya jioni kwa ajili ya wafanyabiashara wadogo.

Sagamiko alisisitiza kuwa maeneo yote  waliyopangiwa wafanyabiashara wadogo katika Manispaa ya Songea kuna miundo mbinu muhimu kama choo, maji na umeme, hivyo basi ifikapo tarehe 30 Oktoba 2021  kila mfanyabiashara awe amehamia kwenye eneo lake na  Ili kuhakikisha wafanyabiashara wadogo hawarejei  kwenye maeneo yasiyo rasmi.

Alisema  Kila Afisa Mtendaji kata, mtaa na Afisa  afya wa Kata watasimamia  maeneo hayo na kuhakikisha wafanyabiashara hao wanaendesha  biashara zao katika maeneo waliyopangiwa na kuwa na  takwimu sahihi za wafanyabiashara wadogo ifikapo tarehe 30/10/2021.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa