• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKURUGENZI ahamasisha wananchi kujitolea

Tarehe ya kuwekwa: May 8th, 2019

MKURUGENZI mtendaji wa wilaya ya Nyasa Jimson Mhagama amewataka wananchi wa Wilaya ya Nyasa kujenga miundombinu ya miradi ya maendeleo kwa kuchangia nguvu zao kuanzia msingi hadi lenta ili kuunga juhudi za Serikali badala ya kuiachia serikali peke yake.

Aliyasema hayo hivi karibuni akiwa katika kata ya lipingo Wilayani hapa akiwa katika ziara ya  kujitambulisha kwa watumishi na wananchi na kukagua ujenzi wa zahanati ya Ngindo iliyopo katika kata hiyo.

Mhagama alifafanua kuwa wananchi wana kila sababu ya kuhakikisha kuwa wanajitoa kwa kuchangia miradi ya maendeleo ili kuwe na maendeleo, na wananchi wakichangia nguvu zao  wanakuwa na uwezo wa kujenga miundombinu na kutatua kero zilizoko katika maeneo yao kwa kuwa inakuwa imeshirikisha jamii.

Aliongeza kuwa wananchi wanatakiwa kuibua miradi ya maendeleo ambayo ni kero katika kata au kijiji na kuanza kujenga hadi kufikia lenta na hatimaye Serikali itaezeka na kununua vifaa vya viwandani na kukamilisha miundombinu hiyo.

Alitoa wito kwa wananchi wa kijiji cha Ngindo kata ya Lipingo kujitoa na kuendeleza ujenzi wa Zahanati ambayo imefikia ngazi ya msingi ili wajenge hadi ngazi ya lenta ndipo Serikali itaweza kukamilisha jengo hilo.

“wanajamii wa kata ya Lipingo tunatakiwa kujitoa kwa kuchangia ujenzi huu wa Zahanati ya Ngindo ambao upo ngazi ya msingi serkali haiwezi kukamilisha kwa hapo mlipofikia,mnatakiwa kuongeza juhudi za hali na mali kwa kuwa serikali iko nyuma yenu. Na mkichangia ujenzi huu hata jamii inakuwa na ari ya kutunza miundombinu hii hata mtu akitaka kuiba dirisha wote mtamzuia lakini ikijenga serikali peke yake hamtakuwa na uchungu wa aina yoyote”.alisema mkurugenzi huyo.

 Alitoa wito kwa wananchi wa kijiji cha Ngindo kata ya Lipingo kujitoa na kuendeleza ujenzi wa Zahanati ambayo imefikia ngazi ya msingi ili wajenge hadi ngazi ya lenta ndipo Serikali itaweza kukamilisha jengo hilo.

Awali Diwani wa Kata ya Lipingo Casbetth Ngwata kwa niaba ya wananchi wa kata hiyo alimuomba Mkururugenzi Mhagama kutatua kero ya ujenzi wa Zahanati ya Lipingo kwa kuwa imekaa kwa muda mrefu bila kuendelezwa ikwa imefika hatua hiyo ya msingi na hamna juhudi zinazofanywa na wananchi katika kuliendeleza jengo hilo.

Wananchi hao waliahidi kujitolea nguvu zao na kuhakikisha jengo hilo linafikia hatua ya lenta ili Serikali iweze kukamilisha na kuanza kutumia Zahanati hiyo ikiwa inalengo la kutatua kero ya wananchi wa kata hiyo kwa kuwa wanalazimika kutembea umbali mrefu kufuata huduma za afya.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa