• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKURUGENZI KUTEMBELEA MRADI WA MACHINJIO YA KISASA MANISPAA YA SONGEA.

Tarehe ya kuwekwa: May 23rd, 2022

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

23 MEI 2022

Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Dkt Frederick Sagamiko amefanya ziara ya kushtukiza na waandishi wa habari katika machinjio ya kisasa iliyopo ndani ya Manispaa ya Songea Kata ya Tanga.

Ziara hiyo ambayo ilifanyika Mei 21, 2022 kwa lengo la kukagua shughuli za uchinjaji wa nyama zinavyofanyika katika machinjio hiyo.

Akizungumza katika ziara hiyo Dkt Sagamiko alisema kuwa mfumo wa uchinjaji nyama katika machinjio hiyo ni wa kisasa ambao unatumia mtambo wa kuchinjia ambapo Manispaa ya Songea ni miongoni mwa miji michache nchini Tanzania ambayo inatumia mtambo huo..

Dkt. Sagamiko aliongeza kuwa kupitia machinjio ya kisasa mapato ya ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea yameongezeka na kuwataka wananchi kutumia nafasi zao mbalimbali kujenga Manispaa ya Songea kwa kuongelea vizuri miradi iliyotekelezwa na namna inavyofanya kazi kwa viwango na ubora unaotakiwa.

Alisema kuwa shughuli za uchinjaji nyama kwenye machinjio hiyo zinasimamiwa na kiongozi wa dini aliyeteuliwa na Baraza la Waislamu Tanzania (BAKWATA) kutoka Mkoa wa Ruvuma na hivyo nyama inayochinjwa katika machinjio hiyo ni halali na inafaa kutumiwa na wananchi wote.

Naye msimamizi wa Machinjio ya kisasa ya Manispaa ya Songea Said Renatus Sangije alisema kuwa machinjio hiyo ina uwezo wa kuchinja Ng’ombe 300 kwa siku ambapo kwa sasa inachinja Ng’ombe 35 hadi 40 tu kwa siku ambao bado hawakidhi mahitaji ya mtambo huo.

Ametoa wito kwa wafanyabiashara wote ndani na nje ya nchi ya Tanzania kutumia fursa hiyo ya machinjio hiyo kwa kuendelea kupeleka Ng’ombe wengi zaidi kuchinja ili kwenda sawasawa na uwezo wa kuchinja wa machinjio hiyo.

Pia, Mchinjaji Mkuu wa Machinjio ya kisasa Shekhe     alieleza kuwa uchinjaji nyama katika machinjio hiyo unazingatia taratibu zote za uchinjaji kwa kuzingatia misingi ya Imani ya Dini ya Kiislamu na kuandaliwa kwa ubora na usafi zaidi.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Tanga Agatoni Michael Goliama alisema kuwa machinjio ya Kisaa ya Manispaa ya Songea imeleta chachu ya maendeleo kwa wakazi wa kata ya Tanga kwa kutoa ajira kwa wananchi wake.

Nao wafanyabiashara wa nyama Manispaa ya Songea wametoa rai kwa wananchi kuendelea kutumia nyama inayochinjwa na machinjio hiyo kisasa kwa kuwa ni safi na salama kwa afya zao.

Mwisho. 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa