• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkurugenzi Manispaa ya Songea Wakili. Muhoja, Amewataka Watumishi Kushiriki Mazoezi

Tarehe ya kuwekwa: November 9th, 2024

Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea, Wakili Bashir Muhoja, amewataka watumishi wa Manispaa ya Songea kutii mamlaka ya viongozi wao, akinukuu maandiko ya Biblia kutoka Warumi 13.

 Wakili Muhoja aliyasema haya wakati wa kufunga tamasha la michezo lililofanyika leo, tarehe 9 Novemba 2024, katika uwanja wa Majimaji.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Wakili Muhoja alimtaka Afisa Michezo wa Manispaa ya Songea, Mohamed Kites, kuunda kikundi cha kufanya mazoezi, ambacho kitajumuisha watu kati ya 40 hadi 50. Kikundi hicho kitakuwa kinafanya mazoezi kila Jumanne, Alhamisi, na Jumamosi kuanzia saa 12 asubuhi kabla ya kuendelea na majukumu ya kazi. Alisema, "Ni muhimu kwa watumishi wetu kuwa na afya bora ili kutimiza majukumu yao kwa ufanisi."

Aidha, Wakili Muhoja alizitaka taasisi mbalimbali kushirikiana na kuendelea kujitokeza kuimarisha afya na kudumisha ushirikiano katika kulitumikia  taifa letu, Aidha,  Aliendelea kusisitiza umuhimu wa mazoezi kwa afya bora na msingi kwa jamii.

Katika hatua nyingine, aliahidi kukutana na walimu wa michezo katika shule mbalimbali ili kuandaa vijana kwa michezo ijayo, akisema kuwa maandalizi bora ndiyo ufunguo wa mafanikio. Alisisitiza kuwa "kila kitu kizuri kina maandalizi yake."

Pia, alitumia fursa hiyo kuwapongeza na kuwatakia heri wanafunzi wanaojiandaa kufanya mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne mwaka 2024, ambao unatarajiwa kuanza tarehe 11 Novemba 2024.

Tamasha la michezo lililofanyika leo lilikuwa ni mwendelezo wa shughuli za kila mwezi za kufanya mazoezi ya viungo, ambazo hufanyika katika wiki ya mwanzo wa kila mwezi.

Imeandaliwa na:
Amina Pilly
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini






Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa